Mwinyi Azindua Miradi ya Maendeleo Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imebuni mfumo mpya wa kupata fedha mbadala ili kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo kwa haraka bila kutegemea fedha za serikali kuu.
Akizungumza Ikulu Zanzibar katika hafla ya utiaji saini wa miradi mikubwa mitatu yenye thamani ya zaidi ya dola milioni 150, ikiwemo ujenzi wa Hospitali ya Saratani Binguni, Dk. Mwinyi alisema hatua hiyo inalenga kuharakisha utekelezaji wa miradi muhimu ya kijamii na kiuchumi. “Tumekuja na wazo la kupata fedha mbadala, limekubalika, na fedha zitaanza kuwasili. Tutalipa bila matatizo yoyote,” alisema Rais Mwinyi.
Alifafanua kuwa awali miradi mingi ilikuwa ikichelewa kutokana na ukosefu wa fedha, lakini sasa serikali imeweka mpango wa akiba wa dola milioni 15 kwa mwezi kwa ajili ya ulipaji wa madeni, ambapo kwa sasa akaunti hiyo imefikia dola milioni 350. Rais Mwinyi alisisitiza kuwa serikali itaendelea kutumia utaratibu huo ili kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa ufanisi na kwa wakati.

Miradi iliyosainiwa ni pamoja na mradi wa mpango mkuu wa matumizi ya ardhi na usajili wa hatimiliki, mradi wa maji safi Mkoa wa Kusini Unguja na ujenzi wa Taasisi ya Saratani Zanzibar. SOMA: Mwinyi ataja sekta 11 kipaumbele awamu ijayo
Mradi wa maji utagharimu uro milioni 56 na unatekelezwa na kampuni kutoka India kupitia ufadhili wa benki ya Ujerumani kwa ushirikiano na CRDB Bank. Utahusisha visima 16, matangi 17 na mtandao wa mabomba wa zaidi ya kilomita 150 utakaonufaisha shehia 34.
Aidha, mradi wa ardhi utagharimu uro milioni 43 na unatekelezwa na kampuni ya IGNFI kutoka Ufaransa kwa ufadhili wa BPI France kupitia CRDB, ukilenga kuanzisha mfumo jumuishi wa taarifa za ardhi na vituo vitano vya huduma za ardhi katika mikoa yote.

Kuhusu Hospitali ya Saratani Binguni, alisema itagharimu dola milioni 32.8 na itatekelezwa kwa ubia na kampuni ya Aegle Onco Care Centre Ltd ya Mauritius. “Hizi changamoto za maji, ardhi na tiba ya saratani ndizo zilikuwa kwenye mawazo yangu. Nashukuru tumepata fedha na sasa tunaanza kazi,” alisema Rais Mwinyi. Dk. Mwinyi alizishukuru wizara na mabenki washirika kwa kushirikiana na serikali katika safari ya maendeleo ya Zanzibar, huku akizitaka taasisi za umma kuondoa urasimu ili miradi ikamilike kwa wakati.




JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
.
This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com
Easy and easy job on-line from home. begin obtaining paid weekly quite $4k by simply doing this simple home job. I actually have created $4824 last week from this simple job. Its a simple and easy job to try to to and its earnings far better than regular workplace job. everyone (nhf-06) will currently get additional greenbacks on-line by simply open this link and follow directions to urge started.
Click On This Link———>>> https://www.Homeprofit1.site
Easy and easy job on-line from home. begin obtaining paid weekly quite $4k by simply doing this simple home job. I actually have created $4824 last week from this simple job. Its a simple and easy job to try to to and its earnings far better than regular workplace job. everyone (nhf-06) will currently get additional greenbacks on-line by simply open this link and follow directions to urge started.
Click On This Link———>>> https://www.Homeprofit1.site