SADC yampongeza Samia ushindi Uchaguzi Mkuu
MAKAMU wa Rais Balozi Dk Emmanuel Nchimbi amesema Serikali inayoongozwa na Rais Dk Samia Suluhu Hassan imechukua hatua za kurejesha utengamano katika nchi na kuhakikisha wananchi wanaishi katika utawala wa sheria.
Makamu wa Rais amesema hayo wakati akimwakilisha Rais Samia katika Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC), uliyofanyika kwa njia ya mtandao, akiwa mkoani Dodoma.

Kwa mujibu wa Taarifa ya Ofisi ya Makamu wa Rais, dhamira ya Rais Samia ni kuhakikisha mchakato wa mazungumzo ya maridhiano unafanikiwa ili kuwa na Taifa lenye amani na umoja na kuendelea kuwa mfano wa utulivu katika Afrika na Dunia kwa ujumla.
SOMA: Waandishi watakiwa kupata taarifa sahihi Uchaguzi Mkuu 2025
Halikadhalika, Makamu wa Rais amesema Tanzania ni salama na tulivu na ipo tayari kuendelea kupokea wageni kutoka duniani kote kwa manufaa ya nchi zote.

Aidha, Makamu wa Rais, amewashukuru viongozi wa SADC walioshiriki uapisho wa Rais Samia pamoja na wote waliotoa pongezi za dhati. Amesema jitihada zote zitatumika kuhakikisha Tanzania inapata maendeleo na amani kuendelezwa.
Mkutano huo umempongeza Rais Samia kwa ushindi aliyoupata na uchaguzi wenye mafanikio.

Mkutano huo ulilenga kujadili kujiondoa kwa nchi ya Madagascar kama nchi Mwenyekiti wa SADC, ambapo nchi ya Afrika Kusini imependekezwa kuwa Mwenyekiti kwa kipindi cha mpito mpaka kufikia mwezi Agosti 2026.
Mkutano huo umekubaliana kuendelea kutumia kauli mbiu ya Mkutano wa 45 wa SADC uliyofanyika nchini Madagascar ambayo ni “Kuimarisha Viwanda, Mapinduzi ya Kilimo, Mabadiliko ya Nishati kwa SADC yenye Uhimilivu”




I get paid over (90$ to 500$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $22000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
.
HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us →→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com