Waumini Waelimishwe Kuhusu Amani

ASKOFU wa makanisa ya PMC Tanzania, Gervase Masanja amesema ni muhimu viongozi wa dini waelimishe waumini waombe amani na utulivu. Askofu Masanja amesema jambo kubwa kwa sasa ni kuendeleza mshikamano ili nchi ipate utulivu na watu waendelee na shughuli za kimaendeleo.
Akizungumza na HabariLEO ofisini kwake Kibaha mkoani Pwani kuwa Watanzania wamejionea hali ilivyokuwa hivyo iwe ni fundisho kuwa amani inapotoweka changamoto zinakuwa ni nyingi. “Falsafa ya 4R inapaswa kupewa nafasi kwani nchi itakuwa salama na iwe ajenda ya kitaifa kwani imegusa kila eneo hivyo ikitumika itasaidia watu kudumisha amani, utulivu na mshikamano wa nchi yetu,” alisema Askofu Masanja.
Ameongeza : “Cha kufanyika kwa sasa ni watu kuliombea taifa kupitia imani zao kwa kushirikiana na viongozi wao ili nchi iweze kurudi kwenye hali yake ya zamani wasikubali kugawanywa ili kulinda amani ya nchi kwani hatuna Tanzania nyingine”. Alisema ni muhimu kuimarisha kamati za ulinzi na usalama za wilaya na mikoa ili zifanye kazi zake vizuri na wananchi wapewe elimu kuhusu mitandao ya kijamii na athari zake.
“Baadhi ya watu walikuwa wakihamasisha maandamano kupitia mitandao ya kijamii tena wengine wakiwa nje ya nchi na kama kuna jambo watumie njia sahihi na si kufanya vurugu,” alisema Masanja. Katibu wa Msikiti wa Hadhara Raji Mzimuni, Maili Moja Kibaha, Mahamudu Mudihiri alisema msingi wa maendeleo unatokana na amani. Mahamudu alisema hata msingi wa imani yoyote unatokana na amani kwa hata neno la Mungu linatufundisha tudumishe amani na mshikamano na utulivu vinatokana na amani na hiyo ni ngao kubwa kwa hatma ya nchi yetu.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Mkoa wa Pwani, Abdala Ndauka alisema falsafa ya 4R itolewe kama waraka ili viongozi na wananchi waweze kuitumia. Ndauka alisema falsafa hiyo imegusa masuala muhimu ya ustawi wa jamii na kiongozi asiyeitekeleza anapaswa ajitathmini kwani atakuwa ameshindwa kutekeleza maelekezo ya Rais. SOMA: Watanzania wahimizwa kupenda nchi, kulinda amani
Amesema kuwa ikienda kama waraka viongozi wataona umuhimu wa kutekeleza tofauti na ilivyo sasa baadhi ya viongozi hawaitekelezi hivyo kushindwa kutatua changamoto za wananchi. Aliongeza kuwa ili amani na utulivu viwepo lazima mahubiri ya upendo na amani yahubiriwe ili kulifanya taifa kuwa na mshikamano ulioasisiwa na waasisi wa Taifa la Tanzania. “Cha kufanyika ni mafundisho ya watu kulinda amani utulivu na kuwa na mshikamano ili nchi iweze kujiletea maendeleo kwani msingi wa maendeleo ni amani,” alisema Ndauka.
Amebainisha kuwa yaliyotokea iwe historia na yasijirudie tena kwani athari zake ni kubwa kwani yamegharimu hasara kubwa na si ya kufanywa na watu wajifunze ili isitokee. Mkurugenzi wa asasi isiyo ya kiserikali ya maendeleo ya vijana ya Kibaha (YPC), Israel Ilunde alisema kuwa huu ndiyo wakati wa kutumia falsafa ya 4R. Ilunde alisema falsafa hiyo inajibu maswali mengi ndani ya nchi na ikitumika vizuri mambo yataenda vizuri na wananchi watakuwa kwenye utaratibu mzuri na kujiletea maendeleo.
Mwenyekiti wa Soko la Loliondo Tangini Kibaha, Mohamed Mnembwe alisema ili watu waweze kufanya shughuli zao wanapaswa kudumisha amani na upendo na mshikamano ili mambo yaende vizuri na waweze kufanya shughuli zao za kila siku. Mnembwe alisema kukiwa na amani na utulivu na mshikamano watu watakuwa na utulivu na watafanya mambo yao bila wasiwasi wowote na watapata maendeleo.




I get paid over (90$ to 500$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $22000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
.
HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us →→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com
Google paid $200 a hour on the internet..my close relative has been without labor for nine months and the earlier month her compensation check was $51005 by working at home for 10 hours a day….. Everybody must try this job now by just use this
Here is I started_____ ⫸ https://Www.Work27.Online
Google paid $200 a hour on the internet..my close relative has been without labor for nine months and the earlier month her compensation check was $51005 by working at home for 10 hours a day….. Everybody must try this job now by just use this
Here is I started___ ⫸ https://Www.Work27.Online
JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
.
This is my main concern……………………. http://www.job40.media