Ajali ya basi yaua 18

TABORA: Watu 18 wamefariki dunia, baada ya basi la abiria kugongana uso kwa uso na lori la mafuta wilayani Nzega, mkoani Tabora.

Kamanda wa Polisi Mkoa Tabora, Richard Abwao, amesema ajali hiyo imetokea leo saa 4 asubuhi eneo la Uchama, Nzega ikihusisha basi la abiria mali ya Kampuni ya Alpha likiwa na abiria 60 wakielekea Dar es Salaam wakitokea jijini Mwanza.

Kamanda Abwao amesema chanzo cha ajali hiyo kwa taarifa za awali zinaeleza ni uzembe wa dereva la lori kutaka kulipita gari lingine bila kuchukua tahadhari.

Ameongeza  kuwa miongoni mwa waliokufa ni wanaume 13, wanawake 5 na wengine 36 wamejeruhiwa  idadi hii ni pamoja na watoto wadogo ambao miili yao ilipelekwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti.

Mkuu wa Wilaya ya Nzega Naitwapwaki Tukai amesema wamepokea miili 18 baadhi yao ni watoto wadogo kwa sasa wanafanya kazi kusaidia majeruhi kupata matibabu yanayohitajika kwa haraka sana iwezekanavyo.

Amesema kuwa serikali wilayani Nzega inafanya kila linalowezekana kuhakikisha matibabu yanapatikana kwa majeruhi wote.

Baadhi ya manusura walikuwa wakipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mji wa Nzega huku wengine wakikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Nkinga wilayani Igunga.

Kwa upande wake, Ofisa Mwandamizi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu (LATRA) Nelson Mmari, amesema kuwa miongoni mwa abiria waliopanda basi hilo lililopata ajali, ni 49 waliokuwa na tiketi za kielektroniki jambo ambalo lilifanya iwe rahisi kutambulika.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Marindsay
Marindsay
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by Marindsay
VickieMinerva
VickieMinerva
1 month ago

★ Join this most wonderful and cool online home based job and start making more than $700 every day. ( t09q) I made $24583 last month, which is incredible, and I strongly encourage you to join and begin earning money from home. Simply browse to this website now for more information.
Click and Copy Here══════►►► http://Www.SmartCareer1.com

Julia
Julia
1 month ago

Every month start earning more than $12,000 by doing very simple Online job from home. I m doing this job in my part time i have earned and received $12,429 last month. I am now a good Online earner and earns enough cash for my needs. Every person can get this Online job pop over here this site.
.
.
Detail Here—————————————————————>>> http://Www.BizWork1.Com

Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x