Akayabangu, vumbi la kongo ni Viagra, zapigwa marufuku

WIZARA ya Afya kupitia Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala limepiga marufuku dawa ya kuongeza nguvu za kiume maarufu Akayabangu.
Taarifa ya Wizara ya Afya iliyosainiwa na Mwenyekiti wa Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala, Profesa Hamis Malebo imesema kuwa dawa hiyo haijathibitishwa na baada ya uchunguzi wamebaini inachanganywa na Viagra.
Amesema, baraza lilipokea taarifa ya uwepo wa dawa hiyo sokoni na hivyo ikafanya uchunguzi wa uingizwaji, usambazaji, ubora na usalama wa kinywaji hicho..
Amesema, baada ya uchunguzi imegundulika kuwa, kinywaji hicho hakijawahi kusajiliwa na Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala.
“Kinywaji hicho cha Akayabangu kimechanganywa na dawa ya kisasa aina ya Sildenafil (Viagra majina mengine Erecto ama Vega) jambo ambalo ni kinyume cha Sheria.”Amesema Profesa Malebo
Amesema kutokana na hali hiyo, hicho siyo kinywaji cha tiba asili bali ni kinywaji chenye viagra.
” Baraza linapiga marufuku uingizaji, usambazaji, uuzaji na utumiaji wa kinywaji hiki kote nchini.
“Yeyote atakayekiuka agizo hilo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake na atakayepatikana akiwa na kinywaji cha Akayabagu, atakuwa ametenda kosa na ataweza kushitakiwa kwa mujibu wa Sheria,” amesema Profesa Malebo.
Aidha, amesema baraza lina tahadharisha umma kuwa makini na matumizi ya dawa ambazo hazijasajiliwa kama Akayabangu na vumbi la kongo kwani dawa hizo hazijapimwa ubora na usalama wake na mamlaka zinazotambulika kisheria.
Amesema pia, kuanzia leo baraza linapiga marufuku uingizaji,usambazaji, uuzaji na utumiaji wa vumbi la Kongo kote nchini.
“Yeyote atakayekiuka agizo hilo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake. Pia ikumbukwe kuwa, yeyote atakayepatikana akiwa na vumbi la Kongo atakuwa ametenda kosa na atashitakiwa kwa mujibu wa Sheria.
“Mtumiaji anayo haki ya kuuliza na kufahamishwa taarifa ya dawa anazopewa kutumia na kuomba kuoneshwa cheti cha usajili wa dawa hizo.
Baraza linaendelea kuikumbusha jamii kuacha tabia ya kutumia dawa hovyo kwani iwapo dawa sio bora na salama, zinaweza kuleta madhara ya kiafya kwa mtumiaji,” amesema Profesa
Im making over $28k a month working part time. I kept hearing other people tell me how much money they can make online so I decided to look into it. Well, p it was all true and has totally changed my life. This is what I do.
AND GOOD LUCK.:)
HERE====)> https://www.salarybiz.com
Home cash earning job to earns more than $500 per day. getting paid weekly morethan $3.5k or more simply doing easy work online. no special skills requiredfor this job and regular earning from this are just awesome. all you need is 2hrs a day for this job and earning are awesome. every person can get this byfollow details here.
.
.
Here►—————————➤ http://WWW.JOIN.HIRING9.COM
Make money online from home extra cash more than $18000 to $21000. Start getting paid every month Thousands Dollars online. I have received $26000 in this month by just working online from home in my part time. every person easily do this job.
….
Open This Website………………>>> http://www.Richcash1.com