Askofu Bagonza aanika ‘sumu’ za maridhiano

ASKOFU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Karagwe, Dk Benson Bagonza ametaja sumu tano zinazoua maridhiano. Amesema hayo wakati wa ibada ya ubarikio wa wachungaji na wadiakonia katika dayosisi hiyo mkoani Kagera.

Ametaja sumu ya kwanza kuwa ni hila na akawaasa watu kujiepusha nayo katika maridhiano. “Wakati mwingine, hila inapewa jina la nia njema au maslahi mapana ya taifa… Tujiepushe na hila kutafuta maridhiano,” alisema Askofu Bagonza.

Pia, amesema watu wanapaswa kujiepusha na kutafuta ushindi katika maridhiano kwa kuwa kuweka mazingira ya kuwa na mshindi kwenye maridhiano huandaa vurugu ya baadaye. “Tatu, kukwepa ukweli, maridhiano yanapatikana endapo ukweli umeonekana hata kama ukweli huo unaumiza pande zote, duniani kote maridhiano hujengwa katika ukweli pasipo kulaumiana,” alifafanua.

Amewashauri wenye madaraka kuyaweka pembeni kwanza na kuingia katika maridhiano na kwamba wahusika wote katika maridhiano huwa kama majeruhi wanaotafuta uponyaji. SOMA: Wasira aahidi kuendeleza maridhiano

Ametaja sumu nyingine kuwa ni kujinufaisha na maridhiano ambapo alisema wanaoongoza maridhiano wasitawaliwe na tamaa ya kutaka kunufaika na wanachojadili au kupendekeza. “Unakuta mtu anapiga kelele za maridhiano lakini anachotafuta ni nafasi baada ya maridhiano, sasa watu wa namna hiyo muwasome na msiwahusishe kwenye maridhiano kwa sababu tayari wana mgongano wa maslahi,” alisisitiza.

Amesema  anaelewa kuwa serikali ina mambo mengi ya kushugulikia lakini maridhiano ya kweli ni jambo la muhimu zaidi Askofu Bagonza alisema mijadala ambayo imekuwepo kuhusu kipi bora kati ya amani na haki kwa sasa si muhimu, hivyo badala yake watu wanapaswa kutambua kila mmoja ni mshindi.

Amesema nje ya maridhiano hakuna uhakika wa nchi kufika inakokwenda kwa sababu taifa lenye manung’uniko ni ngumu kuliongoza hivyo, nchi inahitaji maridhiano kwa gharama yoyote. “Zipo gharama za kisiasa kiuchumi, kijamii na kisera tutatakiwa kuzikubali ili kuipata tena Tanzania tulioizoea, inabidi tupitie gharama chungu kuweza kuipata tena Tanzania tuliyoipoteza iliyotuponyoka katika mikono yetu. Kuna miiko tumeikiuka na dawa yake ni toba, taifa letu ndilo madhabahu yetu tuiheshimu na kuitunza,” alisema Askofu Bagonza.

 

Habari Zifananazo

One Comment

  1. BoT - $34,000,000,000 AVAILABLE KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA MPANGO ELEKEZI 2050 - ANDIKA MRADI SASA NA PATA FEDHA ZA KUSIMAMIA MIRADI NA KUTEKELEZA DIRA 2050 says:

    6.6 PROGRAMU ZA KIELELEZO

    Mpango Elekezi 2050 umeainisha miradi 14 ya kielelezo. Miradi hii inalenga kuleta mageuzi ya viwanda nchini. Pia, itachochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali na uchumi wa kijani. Itasaidia kukuza nguvukazi yenye ujuzi na maarifa ya kisasa. Aidha, miradi hii inalenga kuongeza ushindani wa Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa. Miradi hiyo imepangwa kama ifuatavyo:

    NO PROGRAMME

    1 Mageuzi ya Viwanda kwa Ukuaji wa Uchumi

    2 Ujumuishaji wa Sekta ya Madini kwa Maendeleo ya Viwanda na Uchumi wa Kijani

    3 Ubunifu wa Kidijitali na Miundombinu Mahiri kwa Ukuaji wa Siku za Usoni

    4 Ujenzi wa Uhimilivu wa Tabianchi na Uchumi Endelevu wa Kijani

    5 Kuendeleza Miundombinu na Muunganisho wa Usafiri kwa Tanzania kuwa Kitovu cha Kikanda

    6 Mageuzi ya Sekta ya Nishati kwa Umeme Safi na Endelevu

    7 Kukuza nguvukazi yenye Afya, Elimu na Ujuzi

    8 Kuimarisha Utawala Bora, Uwajibikaji na Mifumo ya Udhibiti

    9 Kuendeleza Miji Mahiri na Miundombinu Endelevu ya Mijini

    10 Kuchochea Biashara, Uwekezaji na Upanuzi wa Uchumi

    11 Kupanua Sekta ya Utalii na Uchumi wa Utamaduni

    12 Kubadilisha Sekta ya Kilimo na Uchumi wa Vijijini

    13 Kuboresha Elimu, Utafiti na Ubunifu wa Kiteknolojia

    14 Mageuzi ya Kifedha ya Kidijitali na Jumuishi .

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button