Azania yaja na mikopo nafuu kwa Watanzania

KATIKA kuendeleza juhudi za Serikali kuboresha maisha ya Watanzania, Benki ya Azania imezindua huduma mbili za mikopo zinazolenga kuwawezesha wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu pamoja na wafanyakazi katika sekta mbalimbali.
Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa huduma hizo “Boom Advance” na “Salary Advance”, Afisa Mwandamizi wa Idara ya Masoko wa benki hiyo, Elizabeth Nyattega, amesema kuwa hatua hiyo ni mwitikio wa mahitaji halisi ya wateja na ni ukombozi mkubwa kwa watumishi wa umma, wafanyakazi wa sekta binafsi pamoja na wanafunzi. SOMA: MAJALIWA: Wizara ya Fedha Walindeni watumiaji wa huduma za fedha
“Benki ya Azania imeendelea kufanya maboresho makubwa katika utoaji wa huduma zake, hatua iliyotupatia tuzo ya Ubora wa Kidijitali Afrika Mashariki 2025 katika tuzo za Africa Bank 4.0 Awards 2025 zilizotolewa na taasisi ya kimataifa ya BII Finance mwaka huu,” alisema Nyattega.

Akifafanua zaidi, Nyattega amesema uzinduzi wa huduma hizo umezingatia mahitaji ya makundi yote nchini, hususan wanafunzi na wafanyakazi. “Kwa wanavyuo na watumishi wote nchini, hii ni fursa kubwa. Sisi kama benki tumehakikisha hakuna sababu ya mtu kukwama,” alisisitiza.
Kuhusu masharti ya mikopo, Nyattega amesema Boom Advance, ambayo inalenga wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu, haitatozwa riba.Aidha, kwa upande wa Salary Advance kwa watumishi wa umma na wafanyakazi wa sekta binafsi, mkopo utatozwa riba nafuu ya asilimia 5 ya mshahara ili kumwezesha mfanyakazi kukidhi mahitaji yake ya kifedha kwa urahisi.




I make up to $90 an hour working from my home. My story is that I quit working at Walmart to work online and with a little effort I easily bring in around $40h to $86h… Someone was good to me by sharing this link with me, so now i am hoping i could help someone else out there by sharing this link…
.
More Details For Us→→→→→→→→→ http://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com