Bashungwa awasili shinyanga kukagua athari za mvua

SHINYANGA: Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amewasili mkoani  Shinyanga kwa ziara ya kikazi ambapo amepokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Christina Mndeme,  Desemba 8, 2023.

Katika ziara hiyo, Waziri Bashungwa atakagua miundombinu ya barabara zilizoharibiwa na mvua kubwa za El-nino zinazoendelea kunyesha katika mkoa huo pamoja na maeneo mbalimbali  nchini.

Advertisement

Miundombinu hiyo iliyoharibiwa na mvua  ni pamoja na barabara ya Shinyanga – Old Shinyanga, barabara ya Old Shinyanga – Solwa, barabara ya Solwa – Kahama na miundombinu mingine ya barabara katika mkoa huo.

 

1 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *