Bil 1/- kudhibiti mafua ya ndege Marekani

SERIKALI ya Marekani imedhamiria kuwekeza Dola bilioni 1 kukabiliana na kusambaa kwa mafua ya ndege, pamoja na kuongeza uagizaji wa mayai kutoka nje ikiwa ni juhudi za kupunguza bei ya bidhaa hiyo.

Taarifa hiyo imetolewa na Waziri wa Kilimo, Brooke Rollins amesema kulingana na takwimu za wizara hiyo zinaonyesha mlipuko huo wa mafua ya ndege umedumu kwa miaka mitatu nakusabababisha kuku milioni 166 kufa tangu 2022.

Aidha amesema virusi hivyo vimeambukiza mifugo 1,000 ya maziwa na watu 70, akiwemo mtu mmoja aliyefariki, tangu mapema 2024.

Katika mkutano na maofisa wa kilimo wa serikali, Waziri Rollins amesema, USDA itatumia hadi Dola milioni 500 kufanya ukaguzi wa usalama wa viumbe kwenye mashamba kwa bure na Dola milioni 400 kuongeza viwango vya malipo kwa wafugaji wanaolazimika kuua kuku wao kutokana na mafua ya ndege.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button