Chalamila arudisha tabasamu kwa Alice

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi Alice Nyamwiza Haule, mjane wa marehemu Justus Rugaibula, hati ya nyumba pamoja na kiasi cha Shilingi milioni 10, baada ya Tume maalum kuchunguza malalamiko ya pande zote mbili na kutoa uamuzi kuwa Alice ndiye mwenye haki ya kupewa nyumba hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar-es-Salaam, RC Chalamila amesema serikali itaendelea kusimamia haki za wananchi endapo zitaonekana kudhulumiwa. SOMA: Chalamila awaonya mabaunsa Dar
Uamuzi huu unakuja kufuatia hatua za awali zilizochukuliwa na RC Chalamila, tarehe Septemba 24, 2025, alipofika kwenye nyumba hiyo na kuagiza Alice Haule pamoja na mfanyabiashara Mohamed Yusufali kufika ofisini kwake kwa mazungumzo.
Lengo la mazungumzo hayo lilikuwa kutafuta suluhu ya amani kati ya pande hizo mbili, baada ya kudaiwa kuwa Alice aliwahi kuvamiwa kwenye nyumba yake namba 3 na watu waliodaiwa kutumwa na Mohamed Yusufali.



