China yafungua milango zaidi kwa Tanzania

ziara ya Chongolo, wajumbe yazaa matunda

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema ziara ya viongozi wake nchini China imezaa matunda kwa kuwa wawekezaji wengi wa taifa hilo watakuja kuwekeza nchini.

Hayo yamesemwa leo Aprili 28 jijini Dar es Salaam na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Sophia Mjema ambaye amesema wawekezaji hao wa  China watawekeza katika sekta ya elimu stadi, kilimo, afya na kubadilishana uzoefu namna China walivyoweza kuondoa umaskini na kuinua uchumi wao.

Amesema kuwa China imeweza kufanikiwa kupitia majimbo matatu na kwamba kama Tanzania ina nafasi ya kufanya mapinduzi ya kimaendeleo sambamba na kuondoa umasikini.

“Rais Samia Suluhu Hassan amefugnua milango ya mahusiano na ushirikiano kimataifa  kwani ziara hii imekuwa na mafanikio  makubwa ambayo  yatakuwa chachu ya kuendelea kuchagiza na kudumisha uhusiano katika nyanja mbalimbali kwa maslahi ya vyama vyetu na wananchi wa nchi zetu mbili.”Amesema  Mjema.

Ziara hiyo ya Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo na wajumbe  20  wa  Halmashauri Kuu na wataalamu wawili  wa chama hicho,  ni utekelezaji wa makubaliano na maelekezo yaliyotolewa na viongozi wakuu, ikiwemo Rais Samia na Katibu wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Xi Jingping.

Mjema amesema viongozi hao walikubaliana  kupandisha hadhi ya uhusiano kati ya CCM  na CPC  kati ya Tanzania na  China kwa kuwa na uhusiano maalumu wa kimkakati  katika nyaja  za elimu na ufundi  stadi, habari  na mawasiliano, kilimo, uvuvi, afya na viwanda.

Amesema kupitia ziara hiyo wamejifunza na na kuona jinsi wenzao walivyoweza kufungua nchi kiuchumi kupitia majimbo ya  Shengzen, Guandong na Guanzhou.

‘’Aprili 17 hadi 28, mwaka huu, Chongolo na  ujumbe wake walitembelea  majimbo  matatu nchini China ambayo  Shengzen, Guandong na Guanzhou katika ziara hiyo.

Pia, walikutana na kufanya mazungumzo na viongozi  mbalimbali wa  CPC Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China  ambao ni, Mkurugenzi wa  Kamisheni ya Mambo ya Nje wa Kamati Kuu ya chama hicho, Wang Yi, Waziri wa Idara  wa Mambo ya  Nje ,Liu Jianchao, wengine ni  Naibu Waziri wa Idara ya Mambo nje, Li Mingxiang , Katibu wa chama hicho jimbo la Hebei, Ni Yuefeng na Mjumbe wa Kamati  ya kudumu ya CPC jimbo la Guandong, Wang Ruijun.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida,  Martha Mlata alisema  walichojifunza China ni jinsi nchi hiyo ilivyowawezesha vijana  kufanya kazi na kujiajiri  maeneo mbalimbali.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button