Mwinyi: Hakuna atakayedhulumiwa fidia

MGOMBEA wa urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameahidi kuunda Tume Maalum itakayofanya tathmini ya kina kuhusu fidia walizolipwa wananchi waliopisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo ya Fumba, Nyamanzi, Dimani na Bweleo, ili kuhakikisha kila mwananchi anapata haki yake stahiki.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Michezo, Dimani, Mkoa wa Mjini Magharibi jana, Dk. Mwinyi alisema tume hiyo itapitia na kuhakiki fidia zote zilizolipwa kwa wananchi kwa lengo la kujiridhisha kuwa kila anayestahiki amelipwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.

Alisema serikali haitamvumilia mtu yeyote atakayebainika kujihusisha na udanganyifu katika michakato ya fidia, ikiwemo wale wanaojenga au kuotesha miti kwa haraka katika maeneo yaliyopangwa kwa miradi ya maendeleo kwa nia ya kudai fidia isiyostahili. “Serikali haitaridhia mtu yeyote kudhulumiwa. Kila anayestahiki atalipwa kwa mujibu wa eneo analomiliki. Lengo letu ni kuwaondoa wananchi katika umasikini, si kuwaingiza katika umasikini,” alisema Dk. Mwinyi.

Aidha, aliagiza Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Masheha kuhakikisha wananchi wanapatiwa elimu kabla ya kutekelezwa kwa miradi yoyote ya maendeleo, sambamba na kupiga picha za maeneo husika ili kuweka kumbukumbu sahihi zitakazosaidia kuepusha migogoro ya ardhi.

Dk. Mwinyi aliwataka wananchi kushirikiana na Serikali katika kudhibiti vitendo vya udanganyifu na wizi wa ardhi, akisisitiza kuwa miradi ya maendeleo inalenga kuboresha maisha ya wananchi, si kuwadhuru. SOMA: SMZ kujenga hospitali mbili za rufaa

Katika mkutano huo, aliomba wananchi kumpa ridhaa ya kuendelea kuiongoza Zanzibar kwa awamu nyingine, ili aweze kukamilisha utekelezaji wa ahadi zake na kuharakisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dk. Muhammed Said Dimwa, alisema chama hakikukosea kumteua Dk. Mwinyi kugombea urais wa Zanzibar, akimwelezea kama kiongozi mzalendo, mtekelezaji wa ahadi na mwenye dira ya maendeleo ya kweli kwa taifa.

Baadhi ya wananchi waliopata nafasi ya kutoa maoni yao walimshukuru Dk. Mwinyi kwa kutekeleza kwa kiwango kikubwa ahadi alizozitoa awali, hatua waliyosema imesaidia kupunguza changamoto nyingi za kijamii katika maeneo yao.

Habari Zifananazo

3 Comments

  1. Google pays $220 an hour online. My close relative had been unemployed for nine months, but last month, she received a $25k paycheck by working from home for 10 hours a day. Everyone should try this job now—just use this link. COPY THIS →→→→ ­­­W­­w­­w­­.S­­a­­l­­a­­r­­y­­­7­­­.­­­Z­­­o­­­n­­­e­­­

    1. I get paid over (90$ to 500$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $22000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
      .
      HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button