Idadi ya wagonjwa saratani kuongezeka duniani

RIPOTI mpya iliyochapishwa na jarida la masuala ya tiba la Lancet inaonyesha idadi ya wagonjwa wapya wa saratani itakua kwa kasi duniani. Wagonjwa wanatarajiwa kuongezeka kutoka milioni 18.5 mwaka 2023 hadi milioni 30.5 mwaka 2050.
Watafiti wa masuala ya afya wanasema ongezeko hili linatokana na jamii kuwa na idadi kubwa ya wazee ambao ni wahanga wakubwa wa saratani. Pia, idadi ya vifo kutokana na saratani inatarajiwa kufikia milioni 10.4, sawa na asilimia 42 ya vifo vyote vilivyotokea mwaka 2023.
Ripoti hiyo pia inaeleza kuwa sababu kubwa za ongezeko la wagonjwa ni matumizi ya tumbaku, ambayo yamesababisha asilimia 21.4 ya vifo vya saratani, hasa katika nchi masikini na zinazoendelea. Ngono isiyo salama pia imesababisha maambukizi ya virusi vya HPV, vinavyosababisha saratani ya shingo ya kizazi.
Ripoti hii ya ongezeko la wagonjwa wa saratani na visababishi vya saratani imehusisha nchi zisizopungua 204 duniani, ikitoa taswira ya kina ya mzigo wa saratani duniani kote. SOMA: Ukaguzi wa mate wapendekezwa kubaini saratani ya tezi dume
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily….
.
More Details For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com