Japan yajitosa kambi ya wakimbizi Nyarugusu

DAR ES SALAAM: SERIKALI ya Japani  imetoa msaada wa  Dola za Kimarekani 500,000  sawa na Sh bilioni 1.250 kwa ajili ya kusaidia wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika kambi ya Nyarugusu mkoani Kigoma.

Balozi wa Japan nchini Yasushi Misawa amekabidhi hundi ya fedha hizo kwa Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) Mahoua Parums.

Misawa amesema nchi yake inatambua umuhimu wa  kulinda haki za binadamu na imekua ikifuatilia changamoto wanazokumbana nazo wakimbizi.

“Kwa niaba ya Serikali ya Japan nawasilisha mchango huu nikiamini kwamba utasaidia kwa kiasi fulani wakimbizi wapya kutoka Kongo kupata huduma za kibidamu zinazohitajika kama  huduma za kiafya, chakula hasa katika kipindi hiki ambacho bei za bidhaa zinazidi kupanda.”Amesema na kuongeza

“Tutaendelea kuunga mkono kazi zinazofanywa na UNHCR na serikali ya Tanzania kufungua milango na kuwasaidia wakimbizi wapya wa Congo katika kambi ya Nyarugusu.”Amesema

Akizungumzia msaada huo, Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) Mahoua Parums amesema kila siku Tanzania inapokea wakimbizi wapya 20 kutoka DRC Congo hadi sasa wapo zaidi ya 250,000 kitu ambacho ameeleza kuwa ni mzigo mzito kwa serikali ya Tanzania.

“Siku chache zilizopita nilikua Kigoma kwenye kambi ya Nyarugusu nikaongea na watoto na wanawake kutoka Congo, nikawauliza mbona wameacha miji yao, kazi zao wamekuja Tanzania, jibu walilonipa ni la kusikitisha, wamekimbia Congo ili kuokoa uhai wao.

“Hakuna anayependa kuwa mkimbizi,niliongea na kina mama wanalia, watoto wapo kwenye mazingira magumu lakini wanacheza wakiwa na matumaini mapya, wapo tayari kwa mapambano.”Amesema

Amesema, zinahitajika Dola milioni 150 kuhudumia wakimbizi waliopo nchini na kuziomba nchi nyingine kusaidia na kusema kuwa ana amini Tanzania itaendelea kufungua milango kwa wakimbizi.

Aidha, amesema fedha zilizotolewa na Japan zitaenda kusaidia kambi ya Nyarugusu kwa kujenga miundombinu kwa ajili ya wakimbizi wapya, vifaa tiba, neti za kuzuia mbu, wataalamu wa saikolojia, chakula na mavazi.

Wakimbizi wapya wanaokimbilia nchini  wakitokea  Kongo tangu Machi 5 mwaka huu,  ni kutokana na ongezeko la mashambulizii ya waasi wa kundi la M23 wanaokabiliana na majeshi ya serikali.

Mkoa wa Kigoma hadi sasa unahifadhi wakimbizi zaidi ya 250,000 kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo na Burundi

 

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
MeghanMarkle
MeghanMarkle
1 month ago

Making extra salary every month from house more than $15,000 just by doing simple copy and paste like online job. I have received $18,000 from this easy home job. Everybody can now makes extra cash online easily.
.
.
Detail Here———————————————————————–>>>  http://Www.BizWork1.Com

Angila
Angila
1 month ago

Start your home business right now. Spend more time with your family and earn. Start bringing 99Dollars per hr just on a computer.(Qj) Very easy way to make your life happy and earning continuously…
.
.
.
This is where i started…>> http://remarkableincome09.blogspot.com

Yvonneearn
Yvonneearn
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by Yvonneearn
Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x