Kadogoo aiomba Serikali kutatua kero ya tembo Mswakini

ARUSHA: Mbunge wa Jimbo la Monduli, Aisack Joseph maarufu ‘Kadogoo’ amemuomba Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Ashatu Kijaji kuingalia kwa jicho la pekee Kata ya Mswakini inayokabiliwa na changamoto ya wanyamapori wakiwemo tembo kuharibu miundombinu ya maji.

Mbunge huyo amesema hayo katika Kata ya Mswakini wakati wa ziara yake ya kuzungumza na wananchi ambapo wananchi hao walidai tembo wanaopita eneo hilo kwenda Hifadhi ya Taifa ya Tarangire na Ngorongoro kuharibu miundombinu ya maji kutokana na bwawa la Nguvu Kazi kujaa tope na kupelekea wanyamapori hao pamoja na mifugo kukosa maji.

Amesema eneo la kata hiyo imepakana na korido ya wanyamapori wanaopita kwenda pia maeneo ya Engaruka lakini kutokana na changamoto ya bwawa hilo kujaa maji wananyapori huharibu mazao ya wananchi na miundombinu ya kisima cha maji kwa kuvunja mabomba.
“Nimepokea kero hii la bwawa la maji kurekebishwa na kuondolewa matope ili wanyamapori wasiharibu miundombinu ya maji hivyo ntawasiliana na waziri husika ili tutatue changamoto hii ili kuzuia wanyama hawa kutoharibu miundombinu ya maji maeneo mengine ya vijiji”

Naye, Diwani wa Kata hiyo Charles Edward ameomba bwawa hilo kutolewa matope ili kuzuia wanyamapori kutoharibu miundombinu ya maji katika kisima cha Naitolia, Laloiboni na Loimarai.



