Kamati ya kudumu ya Bunge Tamisemi yafunguka kituo cha afya Mtwara

MTWARA: Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imeishauri serikali kujenga nyumba za watumishi katika kituo cha afya cha mtandi kilichopo halmashauri ya mji Masasi mkoani Mtwara ili kurahisisha zaidi utoaji huduma kwa wananchi ambapo kimegharimu zaidi ya Sh milioni 500.

Wakizungumza leo Novemba 13, 2023 katika ziara ya siku moja ya kikazi kwa kamati hiyo inayofanyika kwa baadhi ya halmashauri mkoani humo ikiwemo halmashauri ya mji Masasi, Nanyamba mji pamoja na Newala wameeleza kuwa lengo la ziara hiyo kijiridhisha na hatua mbalimbali za utekelezaji wa miundombinu ya afya kwenye sekta hiyo kwenye halmashauri hizo.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga, Salome Makamba amesema hospitali lazima iwe na daktari wa dharura anayeishi jirani na kituo kutokana madaktari wote na wauguzi kuishi mtaani.
“Kwahiyo pamoja na mambo yote ambayo yanafanyika lakini lazima pawe na nyumba ya daktari pamoja na nesi wa dharura kipindi ambacho hospitali inaendelea kufanya kazi”amesema Makamba

Mganga Mfawidhi wa Kituo hicho, Hajirath Mapembe amesema kituo kimeanza kutoa huduma mbalimbali Januari mwaka huu ikiwemo kwa wagonjwa wa nje (OPD), kliniki ya wajawazito na watoto pamoja na zingine.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
EmmaJames
EmmaJames
19 days ago

My last salary was $8,750 only worked 12 hours a week. My longtime neighbor estimated $15,000 and works about 20 hours for seven days. I can’t believe how blunt he was when I looked up his information.
.
.
Detail Here——————————————————>>>  http://Www.BizWork1.Com

Angila
Angila
19 days ago

Making every month extra dollars by doing an easy job Online. Last month i have earned and received $18539 from this home based job just by giving this only mine 2 hrs a day. Easy to do work even a child can get this and start making money Online. Get this today by follow instructions……
.
.
.
On This Website……………..> > W­w­w.S­m­a­r­t­c­a­r­e­e­r­1.c­o­m

Back to top button
2
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x