Gachagua kujadiliwa kesho

KENYA : JAJI wa Mahakama Kuu ya Kenya Chacha Mwita amesema  Mahakama Kuu ya Kenya imeruhusu Bunge la Seneti nchini Kenya kuendelea  kusikiliza hoja ya kumuondoa madarakani Naibu Rais wa Kenya Rigathi Gachagua.

Gachagua aliwasilisha hoja 26 mahakamani kutaka kusitisha kikao cha Seneti kinachotarajiwa kukaa kesho kujadili kuondolewa kwake madarakani lakini sasa kesi hiyo itawasilishwa katika Bunge la kitaifa kwa ajili ya kusikilizwa.

SOMA ” Majaji Kenya kusikiliza kesi ya Gachagua

Advertisement

Hapo kesho, Naibu Rais wa Kenya Rigathi Gachagua anatarajia kujitetea mbele ya seneti  kwa mashtaka yanayomkabili 11 yaliyoidhinishwa na wabunge  282  katika bunge la kitaifa.

1 comments

Comments are closed.