Madereva TZ kushiriki mashindano ya magari Afrika

MOROGORO: MADEREVA 23 kutoka mataifa mbalimbali duniani wakiwemo Watanzania wamethibitisha kushiriki mashindao ya mbio za magari barani Afrika yanayofahamika kwa jina la ‘Mkwawa Rally of Tanzania’ ya umbali wa jumla ya kilometa 338.

Mbio hizo ambayo ni mzunguko wa mwisho wa kuwania ubingwa wa mashindano ya magari Afrika (ARC) (African Rally Championship) yamepangwa kuanzia Septemba 19 na kufikia tamati Septemba 21,mwaka huu mkoani Morogoro.

Msimamizi mkuu wa mashindano hayo, Dk Mosi Makau amesema hayo kuwa tayari madereva 23 wameshajisajili kushiriki , na mashindano hayo ni sehemu ya kuwania Ubingwa wa mashindano ya magari Afrika (ARC).

Amesema kuwa washiriki  wengine wanapambania  kombe la ndani ni baada  ya kufanyika kwa mzunguko  nchini  Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.

Dk Makau amesema mashindano hayo ya mzunguko wa mwisho kwa  mara ya kwanza yanafanyika mkoani Morogoro  ambapo miongoni mwa madereva hao wanagombania taji la Afrika, wapo washindani wa ndani ambao nao wanajiandaa kugombania kombe la ndani la mashindano hayo.

Amesema mashindano hayo ya siku tatu na ufunguzi rasmi utafanyika Septemba 19  mwaka huu , na baada ya ufunguzi tayaendelea eneo la Tungi  (Nanenane ) na Septemba 20  yatafanyika kwenye shamba la Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) eneo la  Mkundi kwa Makunganya na kuwepo kwa hatua tatu .

Dk Makau amesema hatua ya  kwanza itakuwa  mbio za  kilometa 20,  pili ni kilometa  12 na hatua ya tatu ni kilometa 30 na kwmaba kutakuwa na  mizunguko miwili katika kila hatua moja  na mashindano hayo yataendelea siku ya Septemba 21 katika eneo  la  TFS na kufanyika mzunguko mmoja .

“Kwa  siku hizo tatu , jumla ya mashindano yatakuwa ni kilometa 338 , hivyo niwaombe wananchi Mkoa wa Morogoro na Watanzania kwa ujumla  kujitokeza kwa wingi kushuhudia mashindano,”amesema Dk Makau.

Dk Makau amesema mashindano hayo pia ni fursa kwa wakazi na wafanyabishara wadogo wa mkoa huo watafaidika kwa kufanya biashara zao kutokana na   uwingi wa wageni wanaotoka nje ya nchi na  ndani ya nchi kwa ajili ya kuja kushuhudia mashindano hayo.

Naye Mkurugenzi wa magari ya mashindano Tanzania, Satinder Birdi ametaja baadhi ya madereva wa magari 23  wengine ni kutoka  nchi ya Uganda, Rwanda ,Burundi na India  na wote hawa wanaingia Morogoro muda wowote kabla ya kuanza kwa mashindano.

Naye, Mwakilishi wa Mkwawa Group, Emmanuel Mhagama amesema kampuni hiyo imeendelea kushirikiana na Wizara ya Habari ,Utamaduni, Sanaa na Michezo katika kukuza michezo nchini hususan mchezo wa mbio za magari.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mount Uluguru Rally Club, Gwakisa Mahigi ambaye amebeba dhamana ya ulinzi wa mashindano hayo amewataka  wadau na mashabiki wa mchezo huo kufuata maelekezo yatakayotolewa kwa lengo la kulinda usalama wao pamoja na usalama wa mchezo huo.

“Tumeshirikisha wenzetu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama wakiwemo Askari wa Usalama Barabarani, Kikosi cha Kuzuia Ghasia (FFU) na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na kuweka huduma ya kwanza “ amesema Mahigi.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button