Kenya : Maelfu Wamuaga Raila Odinga

MAELFU ya waombolezaji wamefurika katika Uwanja wa Kitaifa wa Kasarani, Nairobi, kutoa heshima za mwisho kwa Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Amolo Odinga, aliyefariki dunia hivi karibuni.Watu wengi kutoka maeneo mbalimbali ya nchi waliokusanyika katika uwanja huo kumuaga kiongozi huyo mashuhuri wa siasa za upinzani.

Viongozi wa kisiasa, kidini na kijamii wamewasili uwanjani hapo wakiwa wamejawa na huzuni, wakimtaja Odinga kuwa shujaa wa demokrasia na mtetezi wa haki za wananchi. Wengi wamesema mchango wake katika mageuzi ya kisiasa nchini Kenya hautasahaulika. SOMA: Ruto ataka Bunge kutafakari hoja za Raila

Mwili wa marehemu ulipokelewa kwa heshima kubwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, kabla ya kusafirishwa kuelekea Kasarani kwa ibada maalumu ya kitaifa. Baadaye, mwili wake unatarajiwa kupelekwa kijijini kwake Kisumu kwa maziko.

 

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button