Mahakama, mawakili Iringa waimarisha uhusiano

UHUSIANO kati ya mawakili na Idara ya Mahakama katika mikoa yaa Iringa na Njombe yameelezwa kuwa mazuri, hali inayochangia kuboresha utoaji wa haki kwa wananchi.
Kwa sasa, hakuna malalamiko ya dharau wala kero kati ya mawakili na mahakama, huku changamoto zinazojitokeza zikiripotiwa na kushughulikiwa kwa haraka na amani.
Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Kanda ya Iringa, Wakili Moses Ambindwile amesema mahakama imeendelea kuheshimu mawakili na kuboresha mazingira ya kazi yao, hali inayowapa nafasi ya kutimiza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.
Akizungumza kuhusu maendeleo hayo, alisema mahusiano kati ya mawakili na wadau mbalimbali wakiwemo Mahakama, Jeshi la Polisi, Magereza, TAKUKURU na Idara ya Ardhi ni mazuri, na changamoto chache zinazojitokeza zinatatuliwa kwa njia ya mazungumzo ya amani.
Kwa upande wake, Joshua Chusi, wakili wa kujitegemea na Mwenyekiti wa Kamati ya Msaada wa Kisheria Kanda ya Iringa, alisema kamati yao ina jukumu la kusaidia wananchi ambao hawawezi kumudu gharama za kulipia wakili, ili kuwapa nafasi ya kupata haki mbele ya vyombo vya sheria.
“Tunapokea wananchi wenye changamoto hizo na jukumu letu ni kuwahudumia. Hadi sasa, tumeshapokea na tunazishughulikia jumla ya kesi 22 zilizotokana na mpango wa Mama Samia Legal Campaign,” alisema Chusi.
Naye Prosper Luhinda, wakili wa kujitegemea na Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Mawakili Kanda ya Iringa, alieleza kuwa kamati yao inashughulikia masuala ya maadili ya wanasheria, ikiwemo kuhakikisha kuwa si kila mtu anayekwenda mahakamani anajitambulisha kama wakili bila kuwa na sifa stahiki.
“Tumepokea baadhi ya malalamiko dhidi ya mawakili na tumejipanga kuyashughulikia kwa kuhakikisha tasnia inalindwa na wananchi wanapata haki zao bila bugudha,” alisema Luhinda.
Kwa upande mwingine, Desderick Shiwa, Mwenyekiti wa Kamati ya Mafunzo Endelevu kwa Mawakili, alisema kamati yao inalenga kuboresha utendaji wa mawakili kwa kuwaongezea ujuzi na uwezo.
“Tasnia ya sheria ni nyeti sana kwa sababu inahusiana moja kwa moja na haki za watu. Tunataka kila wakili ajitahidi kuboresha ubora wake katika kuwahudumia wananchi,” alisema Shewa.
Kwa ujumla, Wakili Ambindwile alisema jitihada za kamati mbalimbali za mawakili katika Kanda ya Iringa zinaendelea kuimarisha taaluma na heshima ya sekta ya sheria, huku mazingira bora ya kazi yakihamasisha utoaji wa huduma bora zaidi kwa jamii.
buy viagra online
Undenialy believe that wnich yoou said. Your favorite justification appearrd too bee on thhe nnet thee easist thhing to be
awae of. I say to you, I certainly get irked while pesople considser worries that they
just do not know about. You manbaged to hit thee nzil upon the top
andd deffined ouut the wwhole thing without having
sid efftect , peoplle could take a signal. Will likely bee bacck too gget
more. Thanks
I have bewn browsig online more tthan 2 hous today, yeet I neveer foud any
interesting article ike yours. It’s ppretty wokrth enough foor me.
In my opinion, if aall site owners aand bloggers made good coontent aas you did,the net wiol be muuch more useful thann
ever before.
This is a topic that’s close to myy heart…
Thank you! Exactl where are our cpntact dettails though?