Mahakama ya juu yagoma kusitisha hukumu ya Trump

MAREKANI : MAHAKAMA ya Juu nchini Marekani imetupilia mbali ombi la Rais mteule Donald Trump la kusitisha hukumu dhidi yake katika kesi ya uhujumu uchumi.
Trump alipatikana na hatia ya kughushi nyaraka ili kuficha malipo ya dola laki 130 kwa muigizaji wa filamu za ngono, Stormy Daniels, kama gharama za kisheria mwaka 2016.
Jaji Juan Merchan, anayesimamia kesi hiyo, alisema hatofikiria kifungo kwa Trump. Majaji wawili wa kihafidhina walijiunga na watatu wa kisoshalisti kumkataa Trump.
Mahakama tatu za New York pia zilikuwa zimekataa ombi la kuchelewesha hukumu, na Mahakama ya Juu imetangaza hukumu itafanyika kama ilivyopangwa Januari 10, 2025, siku chache kabla ya Trump kuapishwa tena kuwa rais. SOMA: Trump kufutiwa mashtaka
Trump alikubaliana kuwa atahukumiwa Julai 2024, lakini mawakili wake walifanikiwa kumshawishi Jaji Merchan kuchelewesha hukumu mara tatu. Hata hivyo, waendesha mashtaka wa Manhattan walikataa ombi la kinga ya rais mteule dhidi ya mashtaka na kuendelea na mchakato wa kisheria.
Uamuzi huu pia unakuja baada ya Trump kushindwa katika mashtaka ya kuingilia uchaguzi wa 2020 na baada ya Mahakama ya Rufaa ya Shirikisho huko Georgia kukataa ombi lake la kuzuia kutolewa kwa ripoti kuhusu njama ya kudhoofisha uhamisho wa madaraka kwa Joe Biden.


