Maji safi, salama Mtwara sasa asilimia 58

KAMPENI ya kumtua mama ndoo kichwani ni moja ya mikakati ambayo imesaidia kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika Wilaya ya Mtwara mkoani Mtwara.
Meneja wa Wakala wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira (RUWASA) Wilaya ya Mtwara Mhandisi Hamisi Masindike amesema hayo wakati akiongea na mwaandishi wa habari hizi ofisini kwake.
“Kampeni ya kumtua mama ndoo kichwani ni moja ya mikakati ambayo imesaidia sana kuongeza upatikanaji wa huduma za maji safi na salama Wilaya ya Mtwara hasa vijijini,” amesema.
Amesema kwa sasa upatikanaji wa maji safi na salama Wilaya ya Mtwara umefikia asilimia 58.
“Upatikanaji wa maji umepanda, wakati RUWASA inaanzishwa 2019 upatikanaji wa maji ulikuwa asilimia 50 lakini kwa sasa tumefikia asilimia 58,” amesema.
Amesema RUWASA Wilaya Mtwara Vijijni ina jumla ya vijiji 197 na kati ya hivyo ni vijiji 52 tu ndivyo havina huduma ya maji safi kufikia sasa.
“Serikali imeweka mipango kuhakikisha vijiji ambavyo havina huduma ya maji ya RUWASA vinapata maji kabla ya kufikia mwaka 2025,” amesema.
Amesema mradi wa Makonde wenye thamani ya Sh bilioni 84 ambao unatekelezwa mkoani Mtwara utatoa huduma ya maji kwa vijiji ambavyo havina maji kwa Wilaya za Newala, Tandahimba, Nanyamba mji ikiwemo vijiji vya Mtwara Vijijini.
Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020 inaelekeza serikali kuhakikisha upatikanaji wa maji umefikia asilimia 85 vijijini na asilimia 95 mijini ifikapo 2025.
Make extra profit every week… this is a great part-time job for everyone… best part about it is that you can work from your home and earn from $100-$2000 each week … start today and have your first payment at the end of the week.
This Website➤—————➤ http://Www.Smartcash1.com
I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com