WAZIRI wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa amesema mapato ya serikali yatokanayo na kodi ya forodha inayokusanywa katika shehena inayopitishwa bandarini yanategemewa kuongezeka kutoka Sh trilioni 7.76 za mwaka 2021/22 hadi Sh trilioni 26.7 mwaka 2032/33.
Vilevile ajira zinazotokana na shughuli za bandari zitaongezeka kutoka 28,990 mwaka 2021/22 hadi ajira 71,907 ifikapo mwaka 2032/33. ⤵️