Mapigano yameanza upya Congo

CONGO :  MAPIGANO yamezuka tena kati ya waasi wa M23 na wanamgambo wanaoungwa mkono na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo huko Mashariki mwa nchi hiyo.

Mapigano haya yamevunja  makubaliano ya usitishwaji wa mapigano ambayo yamedumu kwa wiki kadhaa.

Jumapili ya wiki hii kikundi cha  waasi wa M23 walipambana na wanamgambo wazawa na kuwajeruhi raia 14 wakiwemo vijana wawili.

Advertisement

Usitishaji wa mapigano kati ya jeshi la DRC na waasi wa M23 unaungwa  mkono na Rwanda  kufuatia mazungumzo ya upatanishi yaliyofanyika nchini Angola.

Hapo awali mazungumzo ya  amani kati ya Kinshasa na Kigali yalikwama lakini mazungumzo mengine yamepangwa  kufanyika mjini Luanda mwishoni mwa wiki ijayo.

Tangu M23  ilipoanzisha mashambulizi mapya iliamua kuteka maeneo makubwa yaliyopo mashariki mwa Kongo ambayo yanadaiwa kuwa na utajiri mkubwa  wa madini .

SOMA : DRC Congo na Rwanda kumaliza mapigano