Maziwa yakoleza sumu kwenye viuatilifu-Utafiti

WAKULIMA wametakiwa kutotumia maziwa kama huduma ya kwanza wanapoathiriwa na viuatilifu wakati wa kuvitumia katika mazao shambani au nyumbani.

Angalizo hilo linatokana na kile kilichoelezwa kuwa maziwa yanaipa nguvu sumu hiyo kushambulia seli za mwili wa mwanadamu. Mtafiti kutoka Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu nchini Tanzania (TPHPA), Dk Jones Kapeleka alisema viuatilifu vinapenda kusafiri katika sehemu zenye mafuta kwenye mwili wa mwanadamu.

Kwa kuwa maziwa yana mafuta, inakuwa rahisi kwa viuatilifu kushambulia seli za mwili kupitia katika mafuta kwenda kwenye damu. Alitoa onyo hilo hivi karibuni alipowasilisha matokeo ya utafiti wa athari za matumizi holela ya viuatilifu katika mbogamboga na matunda.

Aliyawasilisha kwenye warsha iliyoandaliwa na Mtandao wa Vikundi vya Wakulima na Wafugaji Mkoa wa Arusha (MVIWAARUSHA), IDP na GAIN kuhusu Mifumo Endelevu ya Chakula kuanzia shambani hadi chakula kinafika mezani.

Dk Kapeleka alisema wakulima wanapoathiriwa na sumu hiyo, kitu cha kwanza wanatakiwa kuwekwa katika sehemu ya wazi yenye upepo wa kutosha kisha kuchukua mkaa na kuusaga na kuuchanganya na maji na kumpa mwathiriwa anywe huku taratibu za kumpeleka hospitali zikiendelea.

“Madhara ya viuatilifu yanatofautiana, kuna ya papo kwa hapo halafu kuna madhara ya muda mrefu, madhara ya papo kwa hapo anayopata mkulima kwanza anatakiwa kuondoka katika mazingira ya viuatilifu, kama amemwagikiwa anapaswa kuoga kwa maji yanayotiririka muda huo huo,” alisema.

Alisema ikiwa mkulima ameathiriwa na kiuatilifu kupitia mdomoni au katika mfumo wa hewa, kitu cha kwanza anatakiwa kuchukuliwa haraka na kuwekwa katika sehemu ya wazi yenye upepo wa kutosha na kunyweshwa mkaa uliopondwapondwa na kukorogwa na maji.

Wakati hayo yakiendelea, utaratibu wa kumpeleka hospitali ufanyike huku chombo cha kiuatilifu kilichomdhuru kikipelekwa pia kwa daktari ili kumfanya atambue aina ya kiuatilifu na matibabu stahiki kwa haraka.

“Sumu za viuatilifu haziondolewi kwa kunywa maziwa kama ilivyozoeleka kwa mtu aliyeathiriwa na dawa, mwathiriwa anatakiwa akorogewe mkaa na apewe anywe lakini si maziwa,” aliongeza.

Alisema kwa watu wanaotumia viuatilifu katika sehemu mbalimbali wanapomaliza kunyunyiza hata kama hawakuathiriwa, wasipendelee kunywa maziwa badala yake wanywe maji kwa sababu ikiwa kuna kiuatilifu kilichojipenyeza mdomoni maziwa yatahatarisha maisha yake.

Habari Zifananazo

13 Comments

  1. I just like the helpful information you provide to your articles. I will bookmark your weblog and take a look at once more here frequently. I am slightly sure I will be informed lots of new stuff proper right here! Good luck for the following!

  2. Thanks for another informative site. The place else may I am getting that type of information written in such an ideal means? I have a project that I’m simply now running on, and I have been at the glance out for such info.

  3. This is really interesting, You’re a very skilled blogger. I have joined your feed and look forward to seeking more of your wonderful post. Also, I’ve shared your web site in my social networks!

  4. Greate pieces. Keep writing such kind of info on your page.
    Im really impressed by your site.
    Hey there, You’ve performed a great job.

    I’ll definitely digg it and personally suggest to my friends.
    I’m sure they will be benefited from this site.

  5. Greetings! This is my 1st comment here so I just wanted to give a quick shout out and tell you I really enjoy reading through your articles. Can you suggest any other blogs/websites/forums that deal with the same subjects? Thanks!

  6. obviously like your website but you have to take a look at the spelling on several of your posts. A number of them are rife with spelling problems and I to find it very bothersome to tell the reality then again I’ll definitely come back again.

  7. Good day! I could have sworn I’ve been to this blog before but after checking through some of the post I realized it’s new to me. Anyways, I’m definitely happy I found it and I’ll be book-marking and checking back frequently!

  8. I’m not sure exactly why but this website is loading incredibly slow for me. Is anyone else having this problem or is it a issue on my end? I’ll check back later on and see if the problem still exists.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button