Mbaroni kwa vipodozi vyenye sumu

JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kuingiza nchini bidhaa za magendo kinyume na sheria ikiwemo vipodozi vyenye viambata vya sumu na mmoja kwa kuingiza nchini trei 48 za mayai ya kuku wa kisasa kutoka Malawi kupitia ‘njia za panya’.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Rashidi Mahenge na Said Suleimani, wote wakazi wa Mji Mdogo wa Tunduma mkoani Songwe pamoja na Furaha George.
Amesema Mahenge na Suleimani walikamatwa katika kizuizi cha polisi eneo la Mwakapangala, Kata ya Nsalala, Mji Mdogo wa Mbalizi, kando ya Barabara Kuu ya Mbeya–Tunduma. Amesema watuhumiwa walikamatwa wakiwa wameingiza nchini vipodozi vyenye viambata vya sumu vilivyopigwa marufuku, makasha 22 pamoja na nyavu za kuvulia samaki zilizopigwa marufuku.

Aidha, walikamatwa wakiwa na vitenge jora 42 bila kibali cha kuingiza bidhaa hizo nchini kutoka Zambia kwa kutumia gari aina ya Toyota Mark X lenye namba za usajili T 371 DSS, mali ya Rashidi Mahenge. Kwa upande wake, Furaha George maarufu kwa jina la Mwakatundu mkazi wa Ipyana wilayani Kyela, amekamatwa kwa tuhuma za kuingiza nchini bidhaa bila kibali.
George alikamatwa eneo la Njiapanda ya Kikusya, Kata ya Itope, wilayani Kyela akiwa ameingiza nchini trei 48 za mayai ya kuku wa kisasa pamoja na sukari kilo 40 kutoka Malawi kupitia vivuko visivyo rasmi. SOMA: Dereva, kondakta washikiliwa usafirishaji vipodozi hatari
Wakati huohuo, polisi mkoani Mbeya wanamshikilia Norasco Mgaya mkazi wa Matembwe mkoani Njombe kwa tuhuma za kupatikana na meno mawili ya tembo. Kwa mujibu wa Kamanda Kuzaga, mtuhumiwa huyo alikamatwa eneo la Mafiati Mbeya akiwa na meno hayo yenye uzito wa kilo 1.6 akiwa ameyafunga ndani ya mfuko wa sandarusi na kuyaficha kwenye begi dogo la mgongoni. Amesema mtuhumiwa alisafiri kutoka mkoani Njombe kwa basi la abiria la Kampuni ya Mwendamseke kutafuta wateja kununua meno hayo, lakini alikamatwa kabla hajatimiza azma yake.




l Get paid over $110 per hour working from home. l never thought I’d be able to do it but my buddy makes over $21269 a month doing this and she convinced me to try. The possibility with this is endless….
This is what I do………………………………….. https://Www.Cash54.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ https://Www.Payathome9.Com