Missenyi waipongeza MSLAC elimu umiliki ardhi

WANANCHI wa vijiji vya Kijumo ,Kitendeguro na Rukurungo kata ya Bugandika wameipongeza serikali  ya kwa  kuleta kampeini ya msaada wa kisheria na kuunda timu inayoongeza uelewa kwa jamii ya wananchi wa vijijini juu ya  maswala ya kisheria hasa yanayohusu ardhi na hati miliki.

Kupitia Kampeini  a msaada wa kisheria inayoendelea wilayani Missenyi kwenye maswala ya kisheria inayoendelea kutolewa jambo kubwa lililowagusa wananchi hao ni kuhusu umuhimu wa kumiliki hati miliki ya ardhi jambo ambalo wamedai kuwa Iinaweza kupunguza migogoro ya ardhi inayoendelea kwa sasa na namna bora ya  kuacha usalama wa familia ni  kuwa na hati miliki ya eneo maeneo yao.

Ofisa ardhi na mipango miji na vijiji wilayani Missenyi  Deliqueen Lyimo akitoa elimu ya kisheria kwa wananchi wa vijiji hivyo alisema kuwa mpango wa Serikali wa wilaya hiyo ni kuhakikisha wananchi wanapata hati miliki za ardhi zao na maeneo wanayoyamiliki ili kuyamiliki kisheria na kupata mikopo ya kufanyia biashara na kujiletea maendeleo.

Akitaja faida za kumiliki hati miliki alisema kuwa changamoto nyingi za ardhi zitapungua, wananchi watapunguza muda wa kwenda mahakamani kugombania ardhi,wananchi watatumia hati zao kuomba mikopo na kujiendeleza kimaendeleo pamoja na kuwasaidia warithi  kutogombania maeneo.

“Mama Samia aliona ni vyema mpate elimu ya kisheria  ili muweze kuondokana na changamoto ndogo ndogo na moja ya maswala ya msingi ni kumiliki  na kuwa na hati na hiyo itawaokoa sana na vijiji vitapata maendeleo sana kupitia hati hizo  na baadhi mnagonbania mipaka  lakini ukipima aridhi yako na kupata hati hautagombana na jirani yako,”alisema Lyimo

Kupitia timu hiyo wananchi wamewaomba wataalamu wa kisheria waliotumwa kutoa msaada wa kisheria kufikisha salamu  kwa Rais Samia kuwa wameipokea kampeini hiyo Kwa mikono miwili  na wamefurahia Elimu na changamoto walizotatuliwa kupitia maswala  ya kisheria  walizotatuliwa

Ponsiani Peter (62) alisema kuwa swala la kumiliki hati miliki za viwanja na maeneo zitapunguza changamoto na malalamiko kwani moja ya changamoto kubwa za kisheria ni kugombania aridhi na wengine wanagombania hata hatua 2 tu ambazo hauwezi kupanda kitu chochote.

Mwenyekiti wa Kijiji Cha Kijumo Roberth  Filederick  alisema kuwa  sasa ni muda wa  vijiji kujianda kupeleka maombi serikalini kwa ajili ya kupima ardhi ili kujipatia maendeleo ambapo amesema kuwa elimu hii ni fursa kwa wananchi wote wa vijijini kwani changamoto ya kutojua sheria inachochea migogoro mingi  hivyo kampeini Hiyo imeleta mwanga mpya   na matumaini mapya kwa wananchi wa vijijini.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button