Mkazi Shinyanga apata suluhisho mgogoro wa miaka mitano

SHINYANGA: MKAZI wa Kijiji cha Bukamba Kata ya Lyabusalu Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Musa Mshindikwa (55) amepata suluhisho kwa kurudishiwa rasilimali zake zilizopotea baada ya kukosa maelewano kwa muda wa miaka mitano tangu alipoanza kuugua marehemu dada yake hadi hatua ya msiba.

Kwani watoto wa marehemu Daudi Washa (43 ) na Sara Bushage (36) walifika mbele ya wataalamu wa msaada wa kisheria nakukiri mjomba wao alimhudumia marehemu kwa makubaliano ya kumlipa fedha Sh milioni 8 alizohudumia msiba wa mama yao.

Mshindikwa amesema hayo leo baada ya kufika kwenye dawati la msaada wa kisheria lililopo Kata ya Iselemagazi halmashauri hiyo nakusikilizwa huku akieleza makubaliano ya awali mbele ya watoto wa marehemu waliafikiana.

Watoa msaada wa kisheria kupitia kampeni ya awamu ya pili ya Mama Samia Legal Aid Mwanasheria Anthony Shakany na Amani Mkwama wamesikiliza changamoto hiyo nakutoa suluhu kwa kuwasikiliza watoto wa marehemu na mjomba wao.

“Watoto wa marehemu wamekubali kumlipa mjomba wao fedha walizokubaliana mbele ya sisi wataalam wa msaada wa kisheria pia tunataka msimamizi wa mirathi kwa mali za marehemu zilizopo sheria ifuatwe,” amesema Shakany.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button