Monaban ateuliwa msaidizi wa askofu mkuu KKAM

ARUSHA: KANISA la Kilutheri Afrika Mashariki (KKAM) limemuingiza kazini Askofu Dk, Philemon Mollel maarufu kwajina la Monaban kuwa msaidizi wa Askofu Mkuu wa kanisa hilo, Oscar Olutu katika Parokia ya Ngulelo jijini Arusha.
Askofu Mollel maarufu kwa jina la Monaban ameingizwa kazini leo katika ibada iliyofanyika katika kanisa hilo eneo la Ngulelo jijini Arusha na kuhudhuriwa na waumini mbalimbali, maaskofu wa kanisa hilo, wachungaji , viongozi wa serikali na wageni waalikwa.

Askofu Mollel aliweka nadhiri kwa kuahidi kutimiza majukumu yote yaliyo mbele yake huku akimuomba mungu amsaidie katika nafaso hiyo ya usaidizi ili aweze kutumika kama kanisa huku maaskofu wengine wakimbariki katika nafasi hiyo ya utumishi wa kanisa
“Mimi askofu Mollel naahidi kuweka nadhiri hii kwa mungu na kuwatumikia waumini wa kanisa hili bila unabaguzi naomba mungu anisaidie katika jukumu hili la kiutumishi”

Kabla ya kumwingiza kazini, Askofu Mkuu Tanzania Kanisa la Kilutheri Afrika Mashariki (KKAM), Oscar Olutu amewasihi waumini wa dini hiyo kutosahau walipotoka huku akisisitiza viongozi wa dini kukiri imani ikiwemo kutokuwa waoga pale wanapohubiri neno la mungu
Askofu Olutu alisema hayo kupitia mahubiri kuwa waumini hao huku akisisitiza wasimpe shetani nafasi ambaye huleta mambo ya uongo bali wamtegemee mungu kwani yeye ndio anayejua imani ya kila mtu kwani katika imani kunajambo linaweza kutokea kupitia imani


