Msifungie watu biashara zao

DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Dk Ashatu Kijaji amezitaka taasisi zote za serikali zinazohusika na ukaguzi na udhibiti kuacha kufungia biashara na viwanda, kwani kufanya hivyo ni kusimamisha uchumi wa nchi.

Kijaji alisema katika maonesho ya wafanyabiashara yaliyoandaliwa na
Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) jijini Dar es Salaam.

“Naomba nisisitize kwa mamlaka zote za serikali za udhibiti ziendelee kuruhusu biashara zifanye kazi hata kama kuna jambo hatukubaliani kati yetu wakati tunashughulikia jambo lile hatuna sababu ya kusitisha kusimamisha shughuli za biashara, ni kusimamisha uchumi wa nchi.

“Kwa hiyo ni muhimu sana tunapoelekea kuhitimisha utekelezaji wetu wa dira yetu ya maendeleo ya mwaka 2025 tusisitishe shughuli yoyote ya kiuchumi kwa jambo lolote lile, kwani mazungumzo ni msingi wa sisi kuwa na uchumi imara, ” alisema.

Alisema Rais Samia Suluhu Hassan, aliamua kuwabeba wafanyabiashara, pia kuwalea wawekezaji wa ndani na nje ya nchi ambao wako ndani ya Tanzania, hivyo mamlaka na taasisi zisifanye mzaha na uamuzi huo.

“Una jambo lako muite muhusika kaa nae acha shughuli ya kiuchumi iendelee kutengeneza ajira kwa vijana wetu kuchangia kukua kwa uchumi wa taifa letu, naamini wamenisikia naomba niwaombe wafanyabiashara na wenye viwanda mliopo hapa na ambao hawapo.

“Nimekabidhiwa jukumu la kuratibu sekta hii, simu yangu iko wazi saa 24 taasisi yoyote ya udhibiti inayokuja kukufungia biashara hata kama ni saa nane usiku nipigie simu tushughulike ili uendelee kufanya kazi,” alisema.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
ShelleDukes
ShelleDukes
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by ShelleDukes
Julia
Julia
1 month ago

For using a home computer to finish some task, I am paid $185 per hour. I had no idea it was feasible, but my close friend convinced me to join her after she earned $25k in just four weeks by performing this difficult work.
.
.
Detail Here—————————————————————–>>>  http://Www.BizWork1.Com

AndiVerna
AndiVerna
1 month ago

★They pay me $285 per hour to work on a laptop. ( z28q) I had no clue it was possible, but a close friend made $26,000 in four weeks working on this simple offer, and she convinced me to try it. For further information, please see.
Click and Copy Here══════►►► http://Www.SmartCareer1.com

Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x