Mwanaume changia damu mara 3 kwa mwaka inaruhusiwa

KATIKA kuadhimisha siku ya kuchangia damu Duniani,Mpango wa Damu Salama, Kanda ya Mashariki umesema mwanaume anaweza kuchangia damu mara tatu kwa mwaka huku mwanamke akiwa na uwezo huo mara nne.
Ofisa Mhamasishaji Mpango huo Kanda ya Mashariki Fatma Mjungu amesema hayo leo Juni 14, 2023 katika kuadhimisha siku ya damu na kuwashukuru wote waliojitokeza kuchangia huduma hiyo kwa ajili ya kuokoa maisha ya wengine.
Amesema hakuna mbadala wa damu na kuchangia kwa ajili ya wahitaji inawezekana kufanya hivyo mara kwa mara.
Kwa upande wake Meneja Mpango wa Damu Salama, Kanda ya Mashariki, Pendael Sifuel amesema mtambo wa apheresis wa kuchakata damu una uwezo wa kuchukua mazao ya damu yanayohitajika kwa mgonjwa, huku damu ikiwa mwilini mwa mchangiaji.
Amesema mazao ya damu yanayoweza kuchakatwa ni pamoja na chembe nyekundu ya damu, plasma na chembe sahani.
Kuhusu mazao ya damu amesema mtambo huo waliokaboidhiwa na serikali una uwezo wa kuchakata damu, huku damu ikiwa mwilini mwa mchangiaji na inatenganisha mazao hayo yad amu kulingana na kiwango kinachohitajika kwa wagonjwa.
“Mwanzoni ilikuwa lazima mchangiaji atoe damu, ambayo mhitaji huwekewa yote kama ilivyo bila kujali mazao yanayotajika katika mwili wake, lakini kwa sasa mashine hiyo imeweza kutenganisha mazao yad amu, huku damu ikiwa mwilini mwa mchangiaji,” amesema Sifuel na kuongeza kuwa mwaka huu wanazindua kadi za kielektroniki kwa wachangiaji damu.
Amesema teknolojia ya kugawa damu kwenye mazao yake ipo kwenye hospitali mbalimbali nchni ikiwemo za mikoa n ahata za rufaa.
Amesema teknolojia hiyo inasaidia badala ya kupewa damu yote halafu mwili ndio uchague kinachitajika kwa sasa, upo uwezekano wa kupewa zao la damu kulingana na uhitaji wa mgonjwa.
Kuhusu maadhimisho amesema hufanyika ili kuwaenzi wale waliochangia damu kwa wagonjwa na kuokoa maisha yao na kwa mwaka huu, walengwa watapewa vyeti vilivyosainiwa na Waziri husika kwa lengo la kuwashukuru.
Amesema kauli mbiu yam waka huu ni pamoja na Changia Damu, haswa mazao yad amu, changia mara kwa mara, ikifafanua kuwa sio kila mgonjwa anayehitaji damu huhitaji damu yote bali wapo wanaohitaji baadhi ya mazao hayo yad amu.
Sifuel amesema kila mchangiaji wad amu anapochangia lazima ichakatwe kulingana na hitaji la mgonjwa na kutolea mfano mgonjwa wa ajali huhitaji zaidi chembe nyekundu yad amu ambayo husaidia hewa ya oksijeni mwilini.
Amesema chembe sahani ya damu husaidia wagonjwa wa saratani ambao wakati mwingine hutokwa na damu bila kuganda hivyo zao hilo husaidia kugandisha damu.