Maisha wenye ulemavu kuboreshwa Z’bar

RAIS wa Zanzibar na Mgombea wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi, amewaomba watu wenye ulemavu nchini kumpa kura katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, huku akiwaahidi kuboresha zaidi maisha yao katika awamu yake ya pili ya uongozi.

Akizungumza na makundi ya watu wenye ulemavu katika ukumbi wa Idriss Abdul Wakil, Kikwajuni – Unguja, Dk. Mwinyi alisema serikali yake tayari imefanya mambo mengi kwa ajili ya kundi hilo, na kwamba wanaweza kutarajia hatua zaidi zitakazoinua ustawi wao endapo atachaguliwa tena.

“Naomba mniunge mkono kwa kunipigia kura tarehe 29 Oktoba. Asibaki mtu nyumbani. Pia tuwaunge mkono wagombea wetu wote wa CCM – kuanzia Dk. Samia Suluhu Hassan, wabunge, wawakilishi hadi madiwani,” alisema Dk. Mwinyi katika mkutano huo uliopambwa na shamrashamra. SOMA: Mwinyi: Hakuna atakayedhulumiwa fidia

Baada ya kusikiliza changamoto mbalimbali zinazowakabili watu wenye ulemavu ikiwemo ukosefu wa ajira, kutoshirikishwa katika ngazi za maamuzi, upungufu wa vifaa saidizi, na miundombinu isiyo rafiki Dk. Mwinyi aliahidi kuchukua hatua madhubuti kuzitatua.

Alisema serikali yake itaendeleza programu za mafunzo, uwezeshaji na mikopo nafuu kwa watu wenye ulemavu, sambamba na kuhakikisha haki zao zote zinalindwa na kutekelezwa ipasavyo. “Sera yetu tayari inataka majengo yote ya serikali na miundombinu izingatie mahitaji ya watu wenye ulemavu. Pia visaidizi kama viti vya magurudumu, mafuta maalum ya watu wenye ualbino, na viungo bandia havina ushuru,” alieleza Dk. Mwinyi huku akishangiliwa.

Akijibu maombi ya kuanzishwa kwa kitengo maalum cha huduma za afya kwa watu wenye ulemavu, Dk. Mwinyi alisema serikali itafungua vituo maalum katika hospitali mpya za Mnazimmoja na Binguni mara tu zitakapokamilika, ili kuhakikisha huduma za matibabu zinapatikana bila ubaguzi au vikwazo vya kifedha.

Vilevile, aliahidi kuongeza nafasi za ajira na uteuzi serikalini kwa watu wenye ulemavu, ili nao washiriki moja kwa moja katika maamuzi na maendeleo ya taifa. Aidha, alisema serikali itaendelea kuimarisha ustawi wa kiuchumi wa kundi hilo kwa kutoa mikopo isiyo na riba na mitaji ya kuendeshea shughuli zao za kiuchumi.

Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Mke wa Rais wa Zanzibar, Mama Mariam Mwinyi; Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo CCM Zanzibar, Khamis Mbeto Khamis; na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dk. Mohamed Said Mohamed Dimwa, ambao walimnadi Dk. Mwinyi.

 

Habari Zifananazo

5 Comments

    1. I get paid over (90$ to 500$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $22000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
      .
      HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com

  1. Earn cash with a job that lets you make more than $700 per day. Get paid weekly with earnings of $3,500 or more by simply doing easy online work. No special skills are required, and the regular earnings are amazing. All you need is just 2 hours a day for this job, and the income is fantastic. Anyone can get started by following the details here:

    COPY THIS →→→→ http://Www.Work99.Site

  2. I get paid more than $100 to $500 per hour for working online. I heard about this job 3 months ago and after joining this I have earned easily 💵$20k from this without having online working skills . Simply give it a shot on the accompanying site…

    Here is I started.→→→→→ https://Www.Works6.Com

  3. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button