NAOT kushirikisha wadau ripoti za ukaguzi

OFISI ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) imesema itaendelea kushirikisha wadau wazielewe ripoti za ukaguzi na kuchangia katika kuimarisha uwajibikaji wa matumizi ya rasilimali za umma. Mchumi Mwandamizi wa NAOT, Emanuel Lazaro amesema hayo alipowasilisha mada kuhusu njia na aina za ukaguzi wakati wa mafunzo ya ukaguzi kwa waandishi wa habari mkoani Morogoro .

Lazaro amesema watu wenye ulemavu wa uoni hafifu wanahitaji ripoti zilizopo kwenye karatasi za nukta nundu na kwamba ofisi hiyo imejielekeza huko kwa kuandaa ripoti ambazo ni za nukta nundu. SOMA: TET yatoa elimu matumizi ya vitabu vya nukta nundu

Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere; Mkaguzi Mkuu wa Nje Mkoa wa Morogoro, Baraka Mfugale amesema mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi.

Mfugale amesema mpango huo unalenga kuimarisha ushirikishaji wadau, hususan vyombo vya habari, katika mchakato wa uwajibikaji wa matumizi ya rasilimali za umma. Mfugale amesema ofisi hiyo imejipanga kuendelea kuboresha uwazi katika utoaji wa taarifa za ukaguzi, kuimarisha mawasiliano na wadau, na kujenga uelewa mpana kuhusu kazi, majukumu na mipaka yake.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Ofisi hiyo, Focus Mauki amesema, ofisi inaamini mafunzo hayo yatawajengea uwezo zaidi wa kuuliza maswali ya kitaalamu, kufanya uchambuzi wa kina na kuibua mijadala chanya inayosaidia serikali, bunge na taasisi nyingine kuchukua hatua stahiki kulingana na mapendekezo ya ukaguzi.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. BoT - $34,000,000,000 AVAILABLE KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA MPANGO ELEKEZI 2050 - ANDIKA MRADI SASA NA PATA FEDHA ZA KUSIMAMIA MIRADI NA KUTEKELEZA DIRA 2050 says:

    6.6 PROGRAMU ZA KIELELEZO

    Mpango Elekezi 2050 umeainisha miradi 14 ya kielelezo. Miradi hii inalenga kuleta mageuzi ya viwanda nchini. Pia, itachochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali na uchumi wa kijani. Itasaidia kukuza nguvukazi yenye ujuzi na maarifa ya kisasa. Aidha, miradi hii inalenga kuongeza ushindani wa Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa. Miradi hiyo imepangwa kama ifuatavyo:

    NO PROGRAMME

    1 Mageuzi ya Viwanda kwa Ukuaji wa Uchumi

    2 Ujumuishaji wa Sekta ya Madini kwa Maendeleo ya Viwanda na Uchumi wa Kijani

    3 Ubunifu wa Kidijitali na Miundombinu Mahiri kwa Ukuaji wa Siku za Usoni

    4 Ujenzi wa Uhimilivu wa Tabianchi na Uchumi Endelevu wa Kijani

    5 Kuendeleza Miundombinu na Muunganisho wa Usafiri kwa Tanzania kuwa Kitovu cha Kikanda

    6 Mageuzi ya Sekta ya Nishati kwa Umeme Safi na Endelevu

    7 Kukuza nguvukazi yenye Afya, Elimu na Ujuzi

    8 Kuimarisha Utawala Bora, Uwajibikaji na Mifumo ya Udhibiti

    9 Kuendeleza Miji Mahiri na Miundombinu Endelevu ya Mijini

    10 Kuchochea Biashara, Uwekezaji na Upanuzi wa Uchumi

    11 Kupanua Sekta ya Utalii na Uchumi wa Utamaduni

    12 Kubadilisha Sekta ya Kilimo na Uchumi wa Vijijini

    13 Kuboresha Elimu, Utafiti na Ubunifu wa Kiteknolojia

    14 Mageuzi ya Kifedha ya Kidijitali na Jumuishi .

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button