Paul Kimiti: Hakuna aliyefanikiwa kwa vurugu

MWENYEKITI wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere, ambaye pia amepata kuwa waziri kwenye wizara mbalimbali nchini,  Paul Kimiti, ameomba Watanzania kuendelea kuenzi na kudumisha urithi wa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, hasa katika kulinda amani na mshikamano wa taifa.

Akizungumza katika mahojiano maalum na Daily News Digital jijini Dar es Salaam, Kimiti amesema Tanzania itaendelea kuwa imara endapo kizazi cha sasa, hususan vijana, kitathamini na kufahamu kuwa nchi ni yao na wanawajibika kuilinda kwa moyo wa uzalendo kama alivyosisitiza Mwalimu Nyerere wakati wa uhai wake.

“Wananchi wetu wajue majukumu yao wanaposikia sera mbalimbali. Hata kama hukubaliani na sera hizo , si suala la kulalama au kupiga kelele. Hilo si suluhisho. “ Ukikubali au hukubali, uamuzi wako una nafasi yake kwenye kura. Mwalimu alitufundisha kuheshimu demokrasia na maamuzi ya wengi, na kufanya fujo hakusaidii kitu chochote,” amesema Kimiti.

Amesema misingi hiyo ya amani, umoja na mazungumzo badala ya vurugu ndiyo siri kubwa iliyoliwezesha taifa la Tanzania kubaki kuwa kisiwa cha amanii Afrika kwa zaidi ya nusu karne tangu kupata uhuru. “Vijana wakitaka wafanikiwe katika maisha yao lazima waelewe nchi ni yao, lazima waipende na wailee. Tukifika mahali ambapo hatuoni umuhimu wa amani, tunajiharibia wenyewe. Hakuna aliyewahi kufanikiwa kupitia vurugu. Wengi wamekosa amani kwa sababu ya kuacha misingi aliyoasisi Mwalimu Nyerere,” ameongeza Kimiti.

Kuenzi alama ya Mwalimu Nyerere

Kauli ya Kimiti imekuja wakati Tanzania ikiadhimisha miaka 26 tangu kufariki dunia kwa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere Oktoba 14, 1999. Katika kipindi chote hicho, Watanzania wameendelea kuenzi mchango wake katika kujenga taifa lenye umoja, amani, usawa na kujitegemea.

Mwalimu Nyerere, kupitia sera yake ya Ujamaa na Kujitegemea, alihimiza wananchi kuwa wamoja na kufanya kazi kwa bidii ili taifa lijitegemee kiuchumi. Alikuwa kiongozi wa mfano, aliyesisitiza maadili, uadilifu na upendo kwa taifa lake. SOMA: Waandishi Bunifu waalikwa kushiriki Tuzo ya Mwalimu Nyerere

Urithi unaodumu vizazi kwa vizazi

Kwa mujibu wa Kimiti, taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere itaendelea kuelimisha vijana kuhusu falsafa na misingi aliyoacha Baba wa Taifa, ili kizazi kipya kijifunze maadili ya uzalendo, uwajibikaji na kuheshimu misingi ya kidemokrasia. “Mwalimu alitupa dira. Ni wajibu wetu kuilinda amani hii kwa vitendo, si kwa maneno. Vijana ndio tegemeo la taifa, wakipotea kwenye vurugu, taifa zima linayumba,” amesema.

Kwa hakika, Mwalimu Nyerere aliweka alama isiyofutika katika historia ya Tanzania na Afrika kwa ujumla alama ya upendo, umoja na amani. Kama alivyoeleza Mwalimu mwenyewe: “Amani haiji kwa bahati, bali ni matokeo ya haki na kuheshimiana.”

Habari Zifananazo

6 Comments

  1. I get paid over (90$ to 500$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $22000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
    .
    HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com

    1. Every month, I earn over $21,000 doing an online job from home in my spare time. Last month, I earned $19,685 from this simple internet business by working just 3 hours a day on my laptop. This work-from-home opportunity is incredible, and the daily earnings far exceed those of typical 9-to-5 desk jobs. Anyone can start earning money online by following the instructions on this website…

      Open this… http://Www.Work99.Site

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com

  3. I honestly didn’t expect much when I first tried this, but here I am making around 6,854/USD a month just by working online a few hours a day from home. It’s not a get-rich scheme, just something steady that’s been working for me quietly in the background. If you’ve been looking for something consistent like I was, here’s what I started with:
    👉 https://www.jobs67.com

  4. Every month start earning more than $12,000 by doing very simple Online job from home.i m doing this job in my part time i have earned and received $12429 last month .I am now a good Online earner and earns enough cash for my needs. Every person can get this Online

    job pop over here this site… ­­ https://Www.Salary7.Zone

  5. I am making a real GOOD MONEY (80$ to 92$ / hr. )online from my laptop. Last month I GOT a check of nearly 21,000$, this online work is simple and straightforward, I don’t have to go to the OFFICE. At that point this work opportunity is for you. If you are interested. Simply give it a shot on the accompanying site link… https://Www.EarnApp1.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button