Rais Mwinyi: Zanzibar ni salama

ZANZIBAR: Rais wa Zanzibar  Dk.

HusseinMwinyi amesema Zanzibar ni salama kwa mtu yoyote, ina amani, umoja, mshikamano na utulivu, kuendelea na  shughuli za kimaendeleo na ibada.

Rais Dk. Mwinyi amesema hayo akizungumza alipojumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika  ibada ya sala ya Ijumaa na kufungua Ijitimai ya Kimataifa Tabligh Markaz Magome ya siku tatu Wilaya ya Chakechake, Mkoa wa Kusini Pemba leo  Februari 2, 2024.

Advertisement

Rais Mwinyi amewataka waumini kuendelea kumuomba Mwenyezi Mungu kudumisha amani, upendo, umoja na mshikamano.

Aidha,  ametoa wito kwa waumini kuwafundisha watoto elimu ya dini ili wawe na hofu ya Mungu kwa kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya, wizi, ubadhirifu wa mali za umma na vitendo vya udhalilishaji .

Pia,  ameipongeza Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar kwa kuratibu vizuri shughuli za dini  kwa utulivu, amani na mshikamano