Rais Samia aagana na Rais wa Romania

RAIS Samia Suluhu Hassan ameagana rasmi na Rais wa Romania, Klaus Werner leo 19 Novemba Ikulu ya Magogoni jijini Dar es salam, baada ya ziara ya siku nne ya kiongozi huyo nchini.
Ziara ya Rais Werner ilikuwa na lengo la kuimarisha ushirikiano katika maeneo ya kimkakati ikiwemo afya, utengenezaji wa dawa, usindikaji wa mazao ya kilimo, madini pamoja na mbinu za kukabiliana na majanga.
Aidha mazungumzo baina yao yamefikia makubaliano ikiwemo kupatikana nafasi 10 kwa ajili ya Watanzania kusoma Romania katika masomo ya udaktari na ufamasi, na Tanzania kutoa nafasi tano za masomo kwa wanafunzi wa Romania kuja kusoma nchini katika vyuo watakavyochagua wenyewe.
Katika ziara hiyo kumekuwepo na uwekaji wa saini wa hati za makubaliano kuhusu kushirikiana katika masuala ya utafiti wa kisayansi katika kilimo na usalama wa chakula pamoja na kukabiliana na majanga.
Sambamba na hayo wamekubaliana kushirikiana katika masuala ya kimataifa ya mikakati ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ambayo itajadiliwa kwa kina kwenye mkutano wa COP28 unaotarajiwa kufanyika Umoja wa Falme za kiarabu mwishoni mwa mwezi Novemba.
Mbunge wa KWANZA MZUNGU KWENYE BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA… KUWAKILISHA HELA ZA WORD BANK, IMF, MISAADA KUTOKA ULAYA… N.K – ZA KUJENGEA BARABARA, RELI, FLYOVER,
file:///C:/Users/User/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image002.jpg
HELA ZAO HAZINA MWAKILISHI – KAMA FUNDI ANAHITAJI NYUMBA YAKE KWA SABABU ALIJENGA YEYE (MCHANGA KANIPA HELA)
I am making $165 an hour working from home. I was greatly surprised at the same time as my neighbour advised me she changed into averaging $195. However, I see the way it works now. I experience masses freedom now that I’m my non-public boss.
.
.
Detail Here——————————————————>>> http://Www.BizWork1.Com