Rais Samia ateua, atengua

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA)
Amemteua Frank Kanyusi kuwa Kabidhi Wasii Mkuu.
Kabla ya uteuzi Frank alikuwa Mwanasheria Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa
Mtwara.

Frank anachukua nafasi ya Angela Kemanzi Anatory ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Pia, amemteua Irene Joseph Lesulie kuwa Naibu Kabidhi Wasii Mkuu.
Kabla ya uteuzi Irene alikuwa Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mashauri ya Kimataifa, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali.
Irene anachukua nafasi ya Lina Robert Sanga ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Zuhura Yunus iliyotolewa leo Juni 11, 2023 imesema uteuzi huo umeanza Juni 8, 2023.