RC Mtanda: Miradi ya Trilioni 5.6 yatekelezwa Mwanza

MWANZA : WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano la kitaifa la ufuatiliaji, tathmini na kujifunza, litakalofanyika jijini Mwanza kuanzia kesho Septemba 10 hadi 13, 2025.

Akizungumza na waandishi mjini  Mwanza , Mtanda amesema ufuatiliaji ni silaha muhimu kwa serikali katika kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa wakati, kwa ubora na kwa thamani halisi ya fedha.  “Kupitia ufuatiliaji na tathmini inayofanyika mara kwa mara kumewezesha utekelezaji wa miradi yenye thamani ya Sh trilioni 5.6 mkoani Mwanza, iliyotolewa na serikali kuu kuanzia mwaka 2021 hadi 2025,” alisema.

Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na Daraja la John Pombe Magufuli, meli ya MV Mwanza, vivuko vipya, hospitali ya hadhi ya kutoa huduma za kibingwa wilayani Ukerewe, soko kuu la kisasa na kipande cha reli ya kisasa cha Mwanza–Kahama. Hatahivyo amesema kongamano hilo litakutanisha washiriki 1,000 kutoka ndani na nje ya Tanzania. SOMA: Naibu Waziri Byabato atoa maelekezo Miradi Mwanza

Habari Zifananazo

13 Comments

    1. Google pays $300 on a regular basis. My latest salary check was $8600 for working 10 hours a week on the internet. My younger sibling has been averaging $19k for the last few months, and he constantly works approximately 24 hours. I’m not sure how simple it was once I checked it out.

      This is my main concern………………. http://Www.Cash43.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button