Salma Kikwete aongoza kwa kishindo

DODOMA: KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa CCM, CPA Amos Makala, ametangaza kuwa Salma Rashid Kikwete ameteuliwa kugombea ubunge Jimbo la Mchinga baada ya kuwa mgombea pekee aliyechukua na kurejesha fomu na kupitishwa.
” Salma Rashid Kikwete alikuwa mgombea pekee aliyechukua fomu Jimbo la Mchinga na amepitishwa akiwa mgombea pekee ,” alisema CPA Amos Makala. SOMA : Majina ya walioteuliwa CCM yanatangazwa
Katika majimbo mengine, Anna Killango Malecela ameongoza kura za maoni Jimbo la Same Mashariki, Hamida Mohammed Abdallah ameibuka kinara Jimbo la Lindi, huku Profesa Joyce Ndalichako akiongoza Jimbo la Kasulu Mjini.



