Serikali yaanika mikakati kudhibiti radi Bukombe

GEITA: SERIKALI imekamilisha kufunga mifumo ya kunasa radi katika shule 12 zilizopo wilayani Bukombe mkoani Geita ikiwa ni sehemu ya kuwalinda wananchi pamoja na wanafunzi dhidi ya ajali za radi.

Hatua hiyo inakuja kufuatia mfululizo wa matukio ya radi wilayani humo ikiwemo tukio la Januari 27, 2025 lililopelekea vifo vya wanafunzi saba na kujeruhi 82 katika shule ya sekondari Businda.

Mkuu wa wilaya ya Bukombe, Pasikasi Muragili ametoa taarifa hiyo katika mahojiano na waandishi wa habari na kueleza kuwa maboresho yanaendelea kabla ya shule kufunguliwa Januari 13, 2026.

Muragili amesema ili kufanikisha mpango huo serikali kupitia halmashauri hiyo imeweka mkakati wa kutenga fedha kidogo kidogo kila mwezi kwa ajili ya uwekaji wa mifumo ya kunasa radi.

Amesema mbali na maeneo ya shule serikali pia imeshatoa maelekezo kwa taasisi za umma na kijamii ikiwemo taasisi za kidini kuchukua hatua ya kuweka mifumo hiyo kwenye maeneo yao.

Amesema ili kufikia malengo serikali wilayani Bukombe inataraji kuanza ukaguzi katika taasisi zote ili kujionea utekelezaji wa suala hilo baada ya muda waliopewa ili kuepuka matukio ya ajali za radi.

“Taasisi zote za umma na kijamii zenye kuwa na watu wengi, tulifanya nao vikao na tulikubaliana na tuliwasisitiza wafanye hivyo,tulipeana muda na kwasasa tunakwenda kuanza ukaguzi”, amesema.

Ifahamike kuwa mkoa wa Geita ni miongoni mwa maeneo ambayo yamekuwa wahanga wa matukio ya ajali za radi ambazo zimetokea kwa miaka ya hivi karibuni hasa maeneo ya shule.

Ikumbukwe, mbali na tukio la shule ya sekondari Businda wilayani Bukombe, pia Oktoba 17,2018 wanafunzi sita wa shule ya msingi EMMACO Vision wilayani Geita walifariki dunia na wengine 23 kujeruhiwa.

Aidha tukio jingine la kusikitisha lilitokea Oktoba 18, 2019 wanafunzi 39 wa Shule ya msingi Ihumilo wilayani Geita walijeruhiwa baada ya kupigwa na radi wakiwa darasani.

Habari Zifananazo

8 Comments

    1. l Get paid over $110 per hour working from home. l never thought I’d be able to do it but my buddy makes over $21269 a month doing this and she convinced me to try. The possibility with this is endless….

      This is what I do………………………………….. https://Www.Cash54.Com

    2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
      .
      M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→→ https://Www.Payathome9.Com

  1. 2. Uma bomba, que pode ser manual ou elétrica, retira o ar do cilindro, montando um vácuo.
    Em casos específicos, como baixos níveis de testosterona, a terapia de reposição hormonal pode ser prescrita.

    O tratamento deve ser de acordo com a causa identificada, como reposição hormonal, interrupção ou troca de medicamentos e terapia sexual.

    Em casos onde a disfunção erétil é causada por níveis baixos de
    testosterona, a terapia de reposição hormonal poderá ser indicada.

    Em alguns casos poderá amparar, porém ainda não é considerado tratamento modelo nessa ocorrência.
    Alguns hábitos de vida aumentam significativamente o
    traço de montar DE. A disfunção erétil (DE) afeta milhões de homens e podes
    comprometer a autoestima, os relacionamentos e a particularidade de vida.
    Agende uma consulta com um urologista e tenha
    mais propriedade de existência sexual. https://diet365.fit/g1-vitaprost-funciona-anvisa-composicao-preco-valor-comprar-resenha-farmacia-bula-reclame-aqui-saiba-tudo-2025/

  2. Write more, thats all I have to say. Literally, it seems as though you relied on the
    video to make your point. You obviously know what youre talking about,
    why waste your intelligence on just posting videos to
    your weblog when you could be giving us something informative to read?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button