Serikali yaeleza mpango kukabili majanga ya moto

DODOMA; SERIKALI imesema mpango wake ni kusambaza magari ya zimamoto na uokoaji kwa wilaya zote nchini kwa ajili ya kukabiliana na majanga ya moto.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Daniel Sillo ametoa kauli hiyo  bungeni leo, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kyerwa, Innocent Bilakwate aliyetaka kujua lini serikali itapeleka gari la Polisi na gari la zimamoto katika wilaya ya Kyerwa  ili kukabiliana na majanga ya moto.

“Serikali kupitia Jeshi la Polisi imepeleka gari jipya moja aina ya Toyota Land Cruiser Pickup kwa Polisi Wilaya ya Kyerwa.

“Aidha kwa upande wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Serikali itapeleka gari moja  katika wilaya hiyo ikiwa ni mpango wa serikali wa kusambaza magari ya zimamoto na uokoaji kwa wilaya zote nchini kwa ajili ya kukabiliana na majanga ya moto.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button