Serikali yaendelea kupambana changamoto ya umeme

LICHA ya upungufu wa maji katika mabwawa ya kuzalisha umeme nchini, serikali imewatoa hofu watanzania ikisema mikakati mbalimbali inaendelea kufanywa katika kukabiliana na adha ya uzalishaji wa nishati hiyo.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk Doto Biteko amesema upungufu huo unashughulikiwa kupitia vyanzo vingine ikiwemo kuongeza kiwango cha gesi kwa ajili ya kuzalisha umeme na matengenezo ya mitambo iliyoharibika.

“Mtaona shida ya umeme imeanza kupungua na katika kipindi kisichozidi miezi sita tutakuwa tumepunguza au kuondoa kabisa tatizo la umeme nchini,” Dk Biteko alisema katika ziara yake aliyoifanya katika bwawa la Mtera kujionea hali halisi ya uzalishaji wa umeme.

Alisema mkakati umewekwa ili kuhakikisha pia maji yaliyopo katika mabwawa yote ya kuzalisha umeme nchini yanatumika kwa uangalifu mkubwa wakati mvua zikisubiriwa kunyesha katika kipindi cha miezi miwili ijayo na kujaza mabwawa hayo.

“Tumekuja kuona hali halisi na kuchukua tahadhari za mapema ambazo ziko ndani ya uwezo wetu na zile zinazoweza kutokea kesho tuweke mipango ya haraka itakayosaidia kupunguza shida ya umeme nchini,” alisema.

Amewataka wananchi kutunza vyanzo vya maji huku akizitaka idara zinazohusika na mazingira kuungana na kuja na mikakati ya ziada itakayookoa vyanzo hivyo.

“Vinginevyo uwekezaji huu na mitambo tunayonunua haitakuwa na maana kama tutaendelea kuharibu vyanzo vya maji,” alisema.

Pia amelitaka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kujenga utaratibu wa kuifanyia matengezo ya mara kwa mara mitambo yake ili kuepukana na adha ya kuharibika ambayo matokeo yake katika uzalishaji wa umeme ni mabaya.

Dk Biteko amesisitiza kwamba kazi ya Wizara ya Nishati ni kuhakikisha wananchi wanapata umeme na akatoa wito kwa Tanesco kutilia mkazo ukarabati wa mitambo yake ili kuepuka matatizo yanayosababishwa na uharibifu huo.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
6 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
MONEY
MONEY
1 month ago

WIZARA YA NDOTO

HOTUBA YA WIZARA YA NDOTO

ULIMWENGU WA NDOTO

One. DEREVA BODABODA ANA NDOTO YA KUMILIKI KAMPUNI YA NDEGE

Two. MUUZA MBOGAMBOGA ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA MBOGA MBOGA

Three. MUUZA VITUNGUU SUMU ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA VITUNGUU SUMU

Four. MUUZA NYANYA ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA NYANYA

Five. MUUZA MAJI ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA NDEGE

Six. MUUZA BAR ANA NDOTO YA KUMILIKI KUJENGA BAR

Seven. MUUZA FREMU ANA NDOTO YA KUMILIKI SHOPPING MALLS

Eight. MGANGA WA KIENYEJI ANA NDOTO YA KUMILIKI HOSPITALI

Nine. MPIGA DEBE ANA NDOTO ZA KUMILIKI KAMPUNI YA MABASI

Ten. MAMA NTILIE ANA NDOTO YA KUMILIKI HOTELS

Eleven. MCHEKESHAJI ANA NDOTO YA KUMILIKI KITUO CHA TELEVISION

Twelve. MTANGAZAJI ANA NDOTO YA KUMILIKI KITUO CHA TELEVISION

Upo sahihi “tukasomeeeeeee tueleweeeeeee Saaaana

Fursa BABA YETU ULIE MBINGUNI NA BWANA YESU ASIFIWE – IMPORT WATU FROM US TO TZ……..

UKIKUTANA NA MZUNGU AKUPE BRIEFCASE YA HELA UTEKELEZE VYOTE MWENYEWE

file:///C:/Users/User/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image002.jpg

Capture.JPG
Work AT Home
Work AT Home
Reply to  MONEY
1 month ago

I make $100h while I’m daring to the furthest corners of the planet. Last week I worked by my PC in Rome, Monti Carlo finally Paris… This week I’m back in the USA. All I do are basic tasks from this one cool site. see it, 
Copy Here→→→→→ http://Www.Smartcash1.com

Last edited 1 month ago by Work AT Home
MONEY
MONEY
1 month ago

WIZARA YA NDOTO

HOTUBA YA WIZARA YA NDOTO

ULIMWENGU WA NDOTO

One. DEREVA BODABODA ANA NDOTO YA KUMILIKI KAMPUNI YA NDEGE

Two. MUUZA MBOGAMBOGA ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA MBOGA MBOGA

Three. MUUZA VITUNGUU SUMU ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA VITUNGUU SUMU

Four. MUUZA NYANYA ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA NYANYA

Five. MUUZA MAJI ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA NDEGE

Six. MUUZA BAR ANA NDOTO YA KUMILIKI KUJENGA BAR

Seven. MUUZA FREMU ANA NDOTO YA KUMILIKI SHOPPING MALLS

Eight. MGANGA WA KIENYEJI ANA NDOTO YA KUMILIKI HOSPITALI

Nine. MPIGA DEBE ANA NDOTO ZA KUMILIKI KAMPUNI YA MABASI

Ten. MAMA NTILIE ANA NDOTO YA KUMILIKI HOTELS

Eleven. MCHEKESHAJI ANA NDOTO YA KUMILIKI KITUO CHA TELEVISION

Twelve. MTANGAZAJI ANA NDOTO YA KUMILIKI KITUO CHA TELEVISION

Upo sahihi “tukasomeeeeeee tueleweeeeeee Saaaana

Fursa BABA YETU ULIE MBINGUNI NA BWANA YESU ASIFIWE – IMPORT WATU FROM US TO TZ……..

UKIKUTANA NA MZUNGU AKUPE BRIEFCASE YA HELA UTEKELEZE VYOTE MWENYEWE

file:///C:/Users/User/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image002.jpg…

Capture1.JPG
MONEY
MONEY
1 month ago

Kuwa mtanzania wa Kwanza kumiliki MAVAZI YA KUELEKEA SAYARI YA MWEZINI 2023 KWA GHARAMA YA SHILINGI 1 TU YA KITANZANIA – KUNA BARAFU SANA

Capture.JPG
MONEY
MONEY
1 month ago

Kuwa mtanzania wa Kwanza kumiliki MAVAZI YA KUELEKEA SAYARI YA MWEZINI 2023 KWA GHARAMA YA SHILINGI 1 TU YA KITANZANIA –KUNA BARAFU SANA

Capture.JPG
MONEY
MONEY
1 month ago

Kuwa mtanzania wa Kwanza kumiliki MAVAZI YA KUELEKEA SAYARI YA MWEZINI 2023 KWA GHARAMA YA SHILINGI 1 TU YA KITANZANIA –KUNA BARAFU SANA..

Capture1.JPG
Back to top button
6
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x