Serikali yasaini mkataba ajira kwa vijana nje ya nchi

DAR ES SALAAM: Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano, imesaini mikataba mitano itakayowawezesha vijana wa Kitanzania kupata ajira nje ya nchi, huku mikataba mingine 16 ikiwa katika hatua za mwisho za kukamilishwa ili kupanua zaidi fursa za ajira kwa vijana.

Hatua hiyo inatajwa kuwa sehemu ya mkakati wa Serikali katika kukuza uchumi na kufanikisha lengo la Taifa la kufikia pato la Dola Trilioni Moja za Kimarekani ifikapo mwaka 2050.
Akizungumza jijini Dar es Salaam Februari 7, 2026, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mheshimiwa Deus Sangu amesema hatua hiyo inaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha vijana wanapata ajira zenye tija ndani na nje ya nchi.

Waziri Sangu ameyasema hayo wakati wa uzinduzi rasmi wa kipindi cha Imbeju Bongo Fursa pamoja na jarida la Mapitio ya Vijana, ambavyo vinalenga kuwawezesha vijana kiuchumi kwa kuwapatia taarifa sahihi kuhusu fursa zilizopo.
Aidha, Waziri Sangu ametumia jukwaa hilo kuiagiza CRDB Bank Foundation kuwazingatia vijana wabunifu waliopo chini ya Baraza la Taifa la Biashara na Maendeleo (NEDC), katika ufadhili wa shilingi bilioni 200 zilizotengwa na Serikali kwa ajili ya kuendeleza bunifu za vijana.

Kwa upande wao, wakieleza umuhimu wa jarida na kipindi cha Imbeju Bongo Fursa katika kuwawezesha vijana kujikwamua kiuchumi, Mkurugenzi wa Baraza la Taifa la Biashara na Maendeleo (NEDC), Bwana Jesse Madauda, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tullyesther Mwambapa, wamesema majukwaa hayo yataongeza uelewa wa vijana kuhusu fursa za kiuchumi na kuwahamasisha kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.





Hi! I could have sworn I’ve been to this site before but after browsing through a few of the articles I realized it’s new to me.
Anyways, I’m certainly pleased I came across it and I’ll
be book-marking it and checking back often!
I just came across this amazing way to earn $6,000-$8,000 a week online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity.
.
Follow Here ……………………… https://Www.Cash54.Com
I get paid over 220 Dollars per hour working from home with 2 kids at home. i never thought i’d be able to do it but my best friend earns over 15k a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life. This is what I do, check it out by Visiting Following Website…
.
More Details For Us→→→→→→→→→ https://Www.Payathome9.Com
I get paid more than $120 to $130 per hour for working online. I heard about this job 3 months ago and after joining this i have earned easily $15k from this without having online working skills.
This is what I do….. www.join.work27.com