Sh bilioni 15 zanufaisha wakulima kila mwaka

DAR E SALAAM: ZAIDI ya Sh bilioni 15 zinatolewa kila mwaka kwa ajili ya kuwasaidia wakulima zaidi ya 600 nchi nzima.

Lengo ni kuendeleza kilimo cha mazao yanayohitajika kwa ajili ya kuzalisha bidhaa za pombe zilizo chini serengeti ikiwa ni katika kusaidia kukuza sekta ya kilimo na biashara.

Mkurugenzi wa Mtendaji wa SBL, Obinna Anyalebechi pamoja na Juanitha Mramba kutoka SBL Tanzania wamesema hatua ya kuwawezeaha wakulima inakwenda sanjari na kuanzisha viwanda vya bia ikiwemo bia ya serengeti inatokana na matunda ya tufaa ikiwa ni utekelezaji wa dira ya 2050 katika upande wa viwanda na ajira m

Aidha, Mramba amesema pa moja na hatua inayopigwa ya kuendeleza viwanda na wakulima bado soko la pombe nchini linakabiliwa na changamoto ya uwepo wa bia zisizo halali ambazo si tu zinaathiri mapato ya kampuni bali mapato ya Taifa pia

Naye Rispa Khatibu pamoja na Flaviana Matata wakiaungumzia bidhaa hiyo wameeleza kuwa imelenga kusaidia kupunguza uagizaji wa bidhaa za bia kutoka nje hasa kipindi hiki huku ikiwa imelenga kutangaza bidhaa za kitanzania kimataifa .

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button