Singida haina pingamizi Gamondi kupewa Stars

DAR ES SALAAM: Klabu ya Singida Black Stars imesema haina pingamizi lolote kwa mamlaka husika endapo Miguel Gamondi atateuliwa kuwa kocha wa kudumu wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, nafasi ambayo kwa sasa anaihudumia kwa muda.

Katika mabadiliko ya kiutendaji yaliyotangazwa leo Jumatatu, Januari 5, 2025 na Bodi ya Wakurugenzi wa klabu hiyo, Gamondi ameondolewa katika nafasi ya ukocha mkuu wa timu na kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa Singida Black Stars.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Gamondi katika nafasi yake mpya atakuwa na dhamana ya kusimamia mipango yote ya kiufundi pamoja na maendeleo ya jumla ya timu kwa lengo la kuimarisha ushindani wa klabu hiyo.

Sambamba na mabadiliko hayo, Singida Black Stars imemtangaza David Ouma kuwa kocha mkuu mpya wa timu hiyo.

Kocha Ouma atasaidiwa na makocha wasaidizi Mousa Nd’aw na Muhibu Kanu, huku benchi hilo jipya likitarajiwa kuanza kazi mara moja.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. l Get paid over $110 per hour working from home. l never thought I’d be able to do it but my buddy makes over $21269 a month doing this and she convinced me to try. The possibility with this is endless….

    This is what I do………………………………….. https://Www.Cash54.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→→ https://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button