Suma JKT yaipiga tafu mama ongea na mwanao

TAASISI ya  Mama Ongea na Mwanao ikiongozwa na Steven Mengere ‘Steve Nyerere) imepokea jozi 500 za viatu kutoka Shirika la uzalishaji mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT) ikiwa ni  kuunga mkono Kampeni ya “Samia Nivishe Kiatu”

Kampeni hiyo inalenga kuwapatia viatu wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari hususani waishio vijijini

Akizungumza jijini Dar Es Salaam leo Novemba 4,2022 Mkurugenzi  Muendeshaji wa kiwanda cha viatu vya ngozi na  uzalishaji mali wa Jeshi la Kujenga Taifa, Meja Mathias Peter John amesema SUMA JKT inaunga mkono kampeni hiyo ya kizalendo ya kusaidia wanafunzi.

“Hatuwezi kusubiri wachina watuvalishie watoto wetu viatu hivyo tumeamua kwa dhati kuunga mkono jitihada zilizoanzishwa na taasisi hiyo kupitia  kwa Mwenyekiti Steven Mengere kuvalisha watoto wa shule za vijijini viatu.”Amesema Meja Mathias na  kuongeza

“Tutahakikisha tunatengeneza jozi za kutosha katika kiwanda chetu na kuwapa thamani watoto wetu.” Amesema

Nae, Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao,  Steven Mengere  ametoa shukrani kwa SUMA JKT  kwa kuona dhamira ya wazi kuungana nao na  kuwasisitiza  wasanii kushirikiana  na jamii inayowazunguka na kuwathamini kwani ni watu ambao wamekua wakinunua kazi za Sanaa zao.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments
Back to top button
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x