Szoboszlai apewa jezi ya Gerrard

ACHANA na Dominik Szoboszlai kujiunga na Liverpool, unaambiwa kiungo uyo raia wa Hungary amekabidhiwa jezi nzito namba 8 iliyokuwa ikivaliwa na nahodha Steven Gerrard.

Szoboszlai amesaini mkataba wa miaka mitano wenye release clause ya €70m.

Baada ya kukamilisha uhamisho huo, Szoboszlai amesema: “Nina tatoo ya Steven Gerrard hiyo ndio sababu ya kwanini alikuwa mkubwa kipindi niko mdogo.

“Klopp? ndio aliniita ni kweli. Nikasema ni sawa, hili jambo litaenda kuwa bora sana na kila kitu kilikuwa sawa.

” amesema Szoboszlai.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button