Taifa Stars katika mtihani kufuzu AFCON leo

TIMU ya Taifa ya soka “Taifa Stars” leo inashuka dimbani katika mchezo wa kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DR Congo.

Mchezo huo wa kundi H utafanyika kwenye uwanja wa Des Martys uliopo mji mkuu wa DR Congo, Kinshasa.

SOMA: Taifa Stars yafuzu Afcon 2023

Advertisement

DR Congo inaongoza kundi hilo ikiwa na pointi 6 baada ya michezo 2 ikifuatiwa na Tanzania pointi 4, Ethiopia pointi 1 na ya mwisho ni Guinea ambayo na haina pointi.

Michezo mingine ya kufuzu AFCON inayopigwa leo ni kama ifuatavyo:

KUNDI E:
Algeria vs Togo

KUNDI F
Ghana vs Sudan

KUNDI J
Burkina Faso vs Burundi