Tanroads Mbeya yaagizwa kumsimamia mkandarasi

SERIKALI imemuagiza Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Mbeya amsimamie mkandarasi anayejenga barabara ya Katumba–Lupaso wilayani Rungwe ili ujenzi huo usisababishe kukatika mawasiliano kwa wananchi.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya ametoa agizo hilo mwishoni mwa wiki wakati wa ziara kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami. SOMA: TANROADS Tabora yarejesha mawasiliano Bukumbi – Kahama
Mradi huo unalenga kuunganisha halmashauri za Busokelo na Rungwe na kuboresha usafiri katika ukanda huo. Barabara hiyo yenye urefu wa zaidi ya kilometa 35.3 inapita katika maeneo ya milimani hali inayosababisha maporomoko ya udongo mara kwa mara na kuifanya kujifunga, jambo linaloathiri mawasiliano na shughuli za kijamii na kiuchumi za wananchi wa Busokelo na maeneo ya jirani.
Kasekenya amewataka wasimamizi wa mradi huo kuhakikisha mkandarasi anatumia fedha alizolipwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo pekee, na si kuzihamishia kwenye miradi mingine, akibainisha kuwa tabia hiyo imekuwa ikichelewesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Meneja wa Tanroads Mkoa wa Mbeya, Suleiman Bishanga amesema barabara hiyo inajengwa kwa gharama ya Sh bilioni 54 na serikali imemlipa mkandarasi fedha za awali Sh bilioni 4.7. Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Jaffar Haniu alisema barabara hiyo ni sehemu ya mradi mkubwa wa Katumba– Lupaso–Mbambo–Tukuyu.
Amemtaka mkandarasi kuwa tayari kuirekebisha wakati wowote itakapojifunga, hasa ikizingatiwa kuwa mvua huanza Desemba na kuendelea hadi Julai.




6.6 PROGRAMU ZA KIELELEZO
Mpango Elekezi 2050 umeainisha miradi 14 ya kielelezo. Miradi hii inalenga kuleta mageuzi ya viwanda nchini. Pia, itachochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali na uchumi wa kijani. Itasaidia kukuza nguvukazi yenye ujuzi na maarifa ya kisasa. Aidha, miradi hii inalenga kuongeza ushindani wa Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa. Miradi hiyo imepangwa kama ifuatavyo:
NO PROGRAMME
1 Mageuzi ya Viwanda kwa Ukuaji wa Uchumi
2 Ujumuishaji wa Sekta ya Madini kwa Maendeleo ya Viwanda na Uchumi wa Kijani
3 Ubunifu wa Kidijitali na Miundombinu Mahiri kwa Ukuaji wa Siku za Usoni
4 Ujenzi wa Uhimilivu wa Tabianchi na Uchumi Endelevu wa Kijani
5 Kuendeleza Miundombinu na Muunganisho wa Usafiri kwa Tanzania kuwa Kitovu cha Kikanda
6 Mageuzi ya Sekta ya Nishati kwa Umeme Safi na Endelevu
7 Kukuza nguvukazi yenye Afya, Elimu na Ujuzi
8 Kuimarisha Utawala Bora, Uwajibikaji na Mifumo ya Udhibiti
9 Kuendeleza Miji Mahiri na Miundombinu Endelevu ya Mijini
10 Kuchochea Biashara, Uwekezaji na Upanuzi wa Uchumi
11 Kupanua Sekta ya Utalii na Uchumi wa Utamaduni
12 Kubadilisha Sekta ya Kilimo na Uchumi wa Vijijini
13 Kuboresha Elimu, Utafiti na Ubunifu wa Kiteknolojia
14 Mageuzi ya Kifedha ya Kidijitali na Jumuishi .