Tanzania yaadhimisha siku ya usafiri majini

DAR-ES-SALAAM : TANZANIA leo imeungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha Siku ya Usafiri Majini Duniani, ambapo Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Mohamed Salum, ametoa wito kwa jamii kulinda mazingira ya bahari.

Amesema kaulimbiu ya mwaka huu “Bahari Yetu, Wajibu Wetu, Fursa Yetu” inakumbusha umuhimu wa bahari katika kutoa ajira, kuchochea uchumi na kuhifadhi uhai wa viumbe majini. SOMA: Mamlaka za usafiri majini Afrika zatakiwa kushirikiana

Amesema shughuli za kibinadamu zimeathiri kwa kiwango kikubwa uwezo wa bahari kutekeleza majukumu yake, akitaja uchafuzi wa plastiki, kumwagika kwa mafuta, kemikali, uvuvi kupita kiasi na ongezeko la hewa ya ukaa kuwa changamoto kubwa. Ameeleza hali hiyo inachangia ongezeko la joto duniani, kupanda kwa maji ya bahari na kuathiri maisha ya jamii nyingi hasa visiwani.

Salum amesisitiza kulinda bahari ni wajibu wa pamoja kwa serikali, sekta binafsi na wananchi. Amesema hatua madhubuti zinahitajika kupunguza uchafuzi, kuhimiza usafirishaji endelevu na kukuza uchumi wa buluu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12000 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..

    HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button